Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, January 2, 2014

Watu watatu wamefariki dunia mkoani Mbeya katika matukio matatu tofauti yaliyotokea mkoani hapa.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi



Watu watatu wamefariki dunia mkoani Mbeya katika matukio matatu tofauti yaliyotokea mkoani hapa.

Tukio la kwanza limetokea majira ya saa tano asubuhi katika Hospitali ya Rufaa Jijini Mbeya ambapo Huruma Laiton[20]mkazi wa Kijiji cha Inyala Kata ya Iyunga kufariki dunia akipatiwa matibabu baada kupigwa na mumewe aitwaye Ezekiel Mwakabenga[21].

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya Ahmed Msangi amesema kuwa chanzo cha mauaji ni wivu wa kimapenzi kwani imedaiwa kuwa marehemu alikutwa akifanya mapenzi na mtu mwingine majira ya saa kumi alfajiri Januari mosi mwaka huu katika nyumba yake.

Mama mwenye nyumba walimokuwa wanaishi wanandoa hao Rose Mwembe baada ya kusikia ugomvi alienda kutoa taarifa kwa Balozi wa mtaa Asajile Kandonga ambapo baada ya kufika na kukuta hali ya marehemu ni mbaya walimkimbiza Hospitali ya Rufaa ndipo alifariki akipatiwa matibabu.

Mtuhumiwa amekatwa na atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika,aidha mwili wa marehemu umezikwa nyumbani kwao Inyala Januari 2 mwaka huu.

Katika tukio la pili Msangi amesema Christopher Myamba[20]mkazi wa Nsalaga ameuwa kwa kuchomwa nakisu shingoni na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ndele,chanzo cha mauaji ni mzozo uliotokea baada ya marehemu na rafiki yake aitwae Baraka Mwalatu kukutana njiani marehemu akiwa na baiskeli Ndele na wenzake walikataa kupisha njia na kumchoma kisu marehemu.

Mtuhumiwa alitoroka mara baada ya tukio na Kamanda Msangi ametoa wito kwa yeyote mwenye taarifa alipo mtuhumiwa akamatwe achukuliwe hatua za kisheria.

Wakati huo ho mtu mmoja aliyefamika kwa jina la Nnanzala Mayala[60] amefariki baada ya kukatwa katwa na vitu vyenye ncha kali na mtu au watu wasiofahamika katka kijiji cha Simike Wilaya ya Mbarali.
Hakuna mtu aliyekamatwa na chanzo cha mauaji hakijafahamika.

No comments: