Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, January 21, 2014

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Vanessa iliyopo Isyesye Jijini Mbeya, Shukrani Gidion, amempa msaada wa vitu mbali mbali Mwanamke Aida Nakawala(25)aliyejifungua watoto wanne kwa mkupuo.

Mkurugenzi wa Shule ya Skondari ya Vanessa iliyopo Isyesye Jijini Mbeya, Shukrani Gidion akimkabidhi Godoro Aida Nakawala mama aliyejifunguwa watoto wanne


Akikabidhiwa maziwa ya watoto

Kushoto ndiye mume wa Aida yaani baba mzazi wa watoto watoto mapacha wanne

Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Vanessa iliyopo Isyesye Jijini Mbeya, Shukrani Gidion akiwa na watoto hao





Mkurugenzi wa Shule ya Sekondari ya Vanessa iliyopo Isyesye Jijini Mbeya, Shukrani Gidion, amempa msaada wa vitu mbali mbali Mwanamke Aida Nakawala(25)aliyejifungua watoto wanne kwa mkupuo.

Akizungumza katika hafla ya kumkabidhi msaada huo iliyofanyika katika Wadi la wazazi katika Hospitali ya Wazazi Meta anakoendelea na matibabu, Mkurugenzi huyo alisema ni jambo la kushangaza kwa binti mdogo kupata watoto wengi katika njia ya kawaida.

Alisema katika maisha yake ameishia kusikia mapacha wawili au watatu lakini Mapacha Wanne imemshangaza sana jambo lililomgusa kumsaidia baadhi ya vitu kulingana na mahitaji ya Mama Wanne ambaye hata hivyo hali yake inaendelea vizuri pamoja na watoto wake.

Vitu alivyotoa ni pamoja na Godoro la futi Tano kwa ajili ya malazi ya watoto baada ya kuruhusiwa kutoka Hospitali, Blanketi, Shuka, Chandarua, Nguo za Mama, Mataulo ya Watoto pamoja na nguo zake,Vifaa vya kunyonyeshea pamoja na Maziwa ya Watoto(lactojeni) ambavyo jumla yake vikigharimu zaidi ya Shilingi Laki tano.

Mkurugenzi huyo awali aliongozana na Waandishi wa Mtandao wa Mbeya yetu ambao mara kwa mara hujitolea kujua hali ya mama huyo pamoja na watoto wake ambapo aliomba kusaidiwa kukabidhi msaada huo ikiwa ni pamoja na kuzunguka madukani ambapo baadhi ya wauza maduka walionekana kuguswa na kujitolea kwa namna mbili ikiwa ni kupunguza bei ya vitu na kutoa nyongeza kwa ajili ya mama.

Hata hivyo Mkurugenzi huyo hakuishia hapo ambapo alichangia fedha ya mafuta kwa Mtandao wa Mbeya yetu uliojitolea kumrudisha Mama huyo nyumbani kwake ambako ni umbali wa Kilomita 150 kutoka Mbeya mjini.

Kwa mujibu wa taarifa za wauguzi katika Hospitali ya Wazazi Meta wamesema hivi sasa Mama huyo hali yake ni nzuri na anaweza kurudi kijijini kwao Chiwanda Wilaya ya Momba Mkoani hapa kutokana na watoto wake kuchangamka.

Aidha Mtandao wa www.mbeyayetu.blogspot.com unaomba kwa Msamaria mwema yoyote atakayeguswa na jambo hili kuchangia fedha ya mafuta kwa ajili ya kufanikisha safari ya mama huyo pamoja na Watoto wake ikiwa ni pamoja na kuhakikisha mahali atakapoishi na watoto hao pana usalama gani.

Na Mbeya yetu

kwa mawasiliano
0754 374408 

1 comment:

Anonymous said...

MWANAMKE HUYO ANAHITAJI MSAADA MKUBWA ZAIDI WA USHAURI WA KUFUNGA KIZAZI KWANI KWA MUJIBU WA HABARI, SASA ANA WATOTO SABA KATIKA UMRI HUO NA WOTE WAKO CHINI YA MIAKA KUMI.