Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, November 19, 2013

MASHINDANO ya mchezo wa vishale (Darts) kitaifa yanatarajia kufanyika Mkoani Mbeya kuanzia Novemba 23 hadi Novemba 24, mwaka huu.

Mwenyekiti wa Darts Mkoa wa Mbeya, Weston Asisya aliyesimama alisema baada ya kupokea mwaliko wa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo kwa mwaka huu kutoka Darts taifa tayari maandalizi ya viwanja yameshakamilika.


katibu wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya, Anna Mwakabonga wapili kushoto  alisema mbali na maandalizi ya kitaifa pia timu ya Mkoa imeandaliwa vizuri kuhakikisha inafanya vizuri ikiwa nyumbani.

Baadhi wa wachezaji wanaounda timu ya Darts Mkoa wa Mbeya, Raymond Mushi alisema mazoezi wanayoendelea kuyafanya pamoja na kikosi kilichoundwa wapinzani wajue watakuja Mbeya kutalii tu.


MASHINDANO ya mchezo wa vishale (Darts) kitaifa yanatarajia kufanyika Mkoani Mbeya kuanzia Novemba 23 hadi Novemba 24, mwaka huu.

Akizungumzia hali ya maandalizi ya michuano hiyo, Mwenyekiti wa Darts Mkoa wa Mbeya, Weston Asisya alisema baada ya kupokea mwaliko wa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo kwa mwaka huu kutoka Darts taifa tayari maandalizi ya viwanja yameshakamilika.

Alisema michuano hiyo itafanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Kiwira iliyopo Jijini Mbeya ambapo jumla ya Mbao za kuchezea 12 zimeshafungwa tayari kwa mashindano.

Alisema Mbeya itakuwa mara ya pili kuandaa mashindano kama hayo kitaifa ambapo mara ya kwanza yalifanyika mwaka 2010 na yalikuwa na mafanikio makubwa hali iliyowavutia kuandaa tena.

Alisema katika mashindano ya mwaka huu yanatarajia kushirikisha mikoa 12 yenye timu za vishale ikiwa na wachezaji zaidi ya 150 Wanawake kwa wanaume ambapo Mkoa wa Mbeya unatakiwa kuandaa timu nne kama mwenyeji.

Alisema kutokana na ukubwa wa Mkoa wa Mbeya wameteua Wilaya ya Rungwe kuwakilishwa kama mkoa ambao utaopaswa kuandaa timu mbili huku Mbeya Mjini nao ukibakia na timu mbili.

Kwa upande wake katibu wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya, Anna Mwakabonga alisema mbali na maandalizi ya kitaifa pia timu ya Mkoa imeandaliwa vizuri kuhakikisha inafanya vizuri ikiwa nyumbani.

Alisema wamejipanga vizuri kuhakikisha timu ya mkoa inaibuka na ushindi mnono tofauti na mashindano ya mwaka jana yaliyofanyika kitaifa Mkoani Mwanza ambapo timu ya Wanawake ya Mkoa wa Mbeya iliibuka kidedea kwa kujinyakulia kombe la mshindi wa pili.

Baadhi wa wachezaji wanaounda timu ya Darts Mkoa wa Mbeya, Raymond Mushi alisema mazoezi wanayoendelea kuyafanya pamoja na kikosi kilichoundwa wapinzani wajue watakuja Mbeya kutalii tu.

Alisema wamejipanga kuhakikisha wanachukua ubingwa katika kila raundi watakayocheza na kwamba wachezaji wengi ni wazoezi na wamecheza vishale kwa muda mrefu hivyo hawaoni sababu ya kushindwa.

Na Mbeya yetu

No comments: