Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, November 12, 2013

JAMII imetakiwa kutowaficha watu wenye ulemavu bali iwajengee uwezo wa kufanya kazi kwa kuwatengea maeneo na siyo kuwaacha wakiwa omba omba mitaani na wengine kufungiwa majumbani.

 Mlemavu wa Viungo, Damas Sanga(48) mkazi wa Igurusi Wilayani Mbarali Mkoa wa Mbeya wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukutwa akiomba msaada katika baadhi ya Ofisi Mkoani Jijini hapa.



JAMII imetakiwa kutowaficha watu wenye ulemavu bali iwajengee uwezo wa kufanya kazi kwa kuwatengea maeneo na siyo kuwaacha wakiwa omba omba mitaani na wengine kufungiwa majumbani.

Rai hiyo imetolewa jana na Mlemavu wa Viungo, Damas Sanga(48) mkazi wa Igurusi Wilayani Mbarali Mkoa wa Mbeya wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukutwa akiomba msaada katika baadhi ya Ofisi Mkoani Jijini hapa.

Sanga alisema si kila mlemavu anastahili kubweteka na kusubiri kupewa misaada na kuomba omba mitaani bali wengine wanauwezo wa kufanya kazi za ujasiliamali kutokana na kuwa na uwezo mkubwa wa kiakili.

Alisema hivi sasa yeye binafsi anauwezo wa kufanya kazi ya ufundi vyuma hivyo ameamua kuomba msaada ili aweze kununua baadhi ya vifaa vitakavyomsaidia katika kazi yake hiyo ili aondokane na kuwa tegemezi kwa kujitafutia riziki yake yeye mwenyewe.

Alivitaja baadhi ya vifaa vinavyohitajika kuwa ni pamoja na Jenereta kubwa, Inveta na Kabwe kwa ajili ya shughuli ya kuchomelea vitu vinavyogharimu Shilingi 390,000 ambapo hadi sasa amefanikiwa kupata shilingi 290,000 alizochangiwa na wasamaria wema hivyo kubakiwa na Shilingi 100,000/= tu.

Mjasiliamali huyo mwenye ulemavu wa miguu alisema hivi sasa anafamilia ya mke mmoja na watoto wanne ambao hawezi kuwahudumia bila kuwa na kazi ya kumwingizia kipato na ndiyo maana anaomba msaada ili aweze kuendesha shughuli zake na kujipatia kipato kitakachoweza kuhudumia familia.

Alisema kwa mtu yeyote atakayeguswa na hali yake awasiliane naye kwa simu namba  0764 036150  au afike nyumbani kwake Shule ya Msingi Igurusi Wilayani Mbarali Mkoani hapa kwa msaada wa hali na mali.

Na Mbeya yetu

No comments: