Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, November 13, 2013

HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA MBEYA: Fastjet yatangaza kuongeza idadi ya safari kati ya Dar na Mbeya

Kampuni ya ndege ya fastjet imetangaza kuwa itaongeza safari zake za anga kati ya Dar na Mbeya kutoka mara tatu kwa wiki hadi kufikia mara saba kwa wiki ifikapo katikati ya mwezi wa disemba.

Kwa mujibu wa taarifa kupitia mtandao wa kampuni hiyo safari za anga kati ya Mbeya na Dar zimekuwa ni maarufu kutokana na idadi kubwa ya abiria na hivyo basi kampuni hiyo imeamua kuongeza safari zake. Kuanzia tarehe 24 Novemba kutakuwa na safari za jumapili na ifikapo tarehe 17 Disemba itaongeza safari nyingine tatu na hivyo kufanya jumla ya safari saba kwa wiki ikimaanisha kila siku ya wiki kutakuwa na safari ya shirika hilo kati ya Dar na Mbeya.

Photo: We are delighted to announce that due to popular demand we are increasing the number of flights on our newly launched Dar es Salaam to Mbeya route! We will now be offering a Sunday flight between the two cities, which will start on Sunday 24th November. In addition to this, from the 17th December, we will begin adding a further three additional flights per week, which means a total of seven fastjet flights per week between Dar es Salaam and Mbeya!

Book your seat now at www.fastjet.com prices start from TSh32,000 one way (exc. tax & charges)Inavyoonekana kuna abiri wengi sana wanaosafiri kati ya mikoa hii miwili kwani hata kampuni ya Precision Air imekuwa na safari za kila siku kati ya Dar na Mbeya na mara nyingi tu imekuwa ikiacha abiria kutokana na ndege hizo kujaa. Pia Tropical Air ya zanzibar ina safari za Mbeya kupitia Dar mara tatu kwa wiki.

1 comment:

Unknown said...

Kwanini hamtaji bei halisi, sijui lolote kuhusu kodi za serikali kwa safari za ndege. Naomba bei kamili ninayotakiwa kuulipa kwa safari huu mwingine ubabaishaji