Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, October 31, 2013

KIKUNDI CHA MSHIKAMANO LUFILYO BUSOKELO CHAZINDUA MLADI WA KUKU


Afisa Kilimo na Mifugo wa Halmashauri ya Busokelo, Gidion Mapunda akizindua mradi wa ufugaji kuku wa kikundi cha mshikamano kilichopo Lufilyo hivi karibuni.


Mwenyekiti wa kikundi cha Ufugaji kuku cha Mshikamano kilichopo Lufilyo Busokelo, Peter Mwandemela akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufanya uzinduzi wa mradi wao.

Baadhi ya viongozi wa kikundi cha Mshikamano na Mgeni rasmi wakibadilishana mawazo ndani ya mradi wa ufugaji kuku muda mfupi baada ya kuzinduliwa.



Kuku wapatao 100 wanaomilikiwa na kikundi cha Mshikamano kilichozinduliwa, kuku ambao hutaga mayai zaidi ya 70 kila siku wakiwa ndani ya banda lililojengewa kwa mianzi inayopatikana kiurahisi kijijini hapo.

IMEELEZWA kuwa njia rahisi ya kupunguza umaskini kwa jamii ya Watanzania ni kuwahamasisha wananchi kujikita katika miradi ya ufugaji wa kuku, kwa kile kilichodaiwa kutokuwa na gharama kubwa.

Hayo yalibainishwa na Afisa Kilimo na Mifugo wa Halmashauri ya Busokelo,Gidion Mapunda wakati wa uzinduzi wa Mradi wa ufugaji Kuku wa Kikundi cha Mshikamano katika sherehe zilizofanyika juzi katika viwanja vya ofisi za kikundi hicho zilizopo kata ya Lufilyo Wilayani Rungwe Mkoa wa Mbeya.

Mapunda alisema mradi wa kuku ni rahisi sana kuendeshwa na kila mwananchi endapo atahamasishwa kufuga kuku kwa kutumia rasilimali zinazomzunguka kwa kujengea mabanda ya kawaida ambayo yanaweza kumkomboa kiuchumi na hatimaye kupunguza wimbi la umaskini miongoni mwa jamii.

“ kila mtu aanze kufuga kuku nyumbani kwake na siyo lazima kujenga mabanda ya kisasa tumieni rasilimali zinazowazunguka ambazo ni rahisi kuzipata bila gharama yoyote lakini matunda yake yatakuwa makubwa baada ya kuanza kuvuna mayai” alisema Afisa huyo.

Aliongeza kuwa mbali na mradi wa ufugaji kuku kuwa rahisi kuendeshwa na kila mtu pia kunachangamoto ya upatikanaji wa madawa ya kinga ya mifugo inayotokana na kufungwa kwa kiwanda kilichokuwepo Nchini hivyo kutegemea madawa kutoka nje ya nchi ambayo ni gharama kuhifadhi.

Alisema ili kuepukana na magonjwa nyemelezi kwa mifugo ni bora wananchi na wafugaji wakazingatia usafi wa mabanda wa mara kwa mara hali itakayosaidia kuepusha magonjwa yasiyokuwa ya lazima kwa mifugo hususani Kuku wanaoathirika zaidi na ugonjwa wa kideli.

Awali akisoma Risala mbele  ya mgeni rasmi na wageni waalikwa, Katibu wa Kikundi cha Mshikamano, Nikutusya Sakujonga alisema kikundi kilianzishwa Mwaka 2011 na sasa kina kuku wapatao 100 ambao wameanza kutaga hivyo kikundi hukusanya mayai zaidi ya 70 kwa siku.

Alisema wakati kikundi kinaanzishwa kilikuwa na wananchama 20 lakini hadi sasa wamebakia 10 kutokana na wengine kuhama makazi katika kata hiyo na kuhamia maeneo mengine ambapo  Wanaume wako watano na wanawake wako watano ambao wanawakilishwa vitongoji tofauti.

Aliongeza kuwa kikundi kilianza na mtaji wa shilingi 100,000/= lakini sasa mtaji unazidi kukua na kufikia shilingi Milion 4,500,000/= pamoja na kujiunga na chama cha kuweka na kukopa Saccos.

Katibu huyo alisema chama kinamatarajio mengi sana ambapo aliyataja moja wapo kuwa ni kununua mashine ya kukoboa na kusaga nafaka ambayo itasaidia upatikanaji wa chakula cha kuku, kununua mashine ya kutotoreshea vifaranga, kusomesha watoto yatima na kumwezesha kila mwanakikundi kuwa na mradi wake binafsi.

Aidha alitoa shukrani kwa Serikali ya Mkoa wa Mbeya kwa kukipatia kkikundi hicho mizinga 10 ya Nyuki  pamoja na Asasi ya Elimisha ambayo ndiyo iliyotoa elimu kwa wananchi wa Kata ya Lufilyo kujiunga katika makundi na kufungua miradi elimu ambayo imezaa matunda kwa kuanzishwa kwa kikundi cha Mshikamano na kuwa na mradi mkubwa wa ufugaji wa kuku.

Na Mbeya yetu

No comments: