Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, October 31, 2013

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Mtoto Joshua Isack (4) aliyepotea nyumbani kwao akiwa anacheza na watoto wenzie kwa siku tatu akutwa akiwa amefariki dunia ndani ya shimo la choo cha jirani na kuzua maswali ya sintofahamu kwa wazazi na majirani.

Mwili wa Mtoto Joshua Isack (4) ukichukuliwa na polisi
Hili ndilo shimo alimokutwa  marehemu Joshua




KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida Mtoto Joshua Isack (4) aliyepotea nyumbani kwao akiwa anacheza na watoto wenzie kwa siku tatu akutwa akiwa amefariki dunia ndani ya shimo la choo cha jirani na kuzua maswali ya sintofahamu kwa wazazi na majirani.

Tukio hilo la kuonekana kwa mtoto huyo lilitokea jana majira ya saa Kumi jioni katika Mtaa wa Nyibuko Pambogo kata ya Iyela Jijini Mbeya baada ya juhudi za wazazi na majirani kushirikiana kumtafuta na kumpata akiwa amepoteza maisha ndani ya shimo la choo.

Akizungumza kwa uchungu na masikitiko makubwa baba mzazi wa marehemu Isack Daniel ambaye ni mfanyakazi wa Mamlaka ya Maji Mbeya alisema Mtoto wake huyo wa kiume alikuwa anacheza na wenzie jumatatu ya Oktoba 28,  majira ya saa 12 jioni lakini alitoweka katika mazingira ya kutatanisha.

Alisema baada ya kuona giza linaingia na mtoto hajarudi alianza kumtafuta katika kila eneo akishirikiana na baadhi ya ndugu na majirani lakini hakufanikiwa kumwona kwa siku hiyo ambayo kesho yake akiwa ni viongozi wa mtaa walienda kutoa taarifa kituo cha Polisi cha Kati Mbeya Mjini.

Mzazi huyo aliendelea kusema baada ya kutoa taarifa polisi bado waliendelea na juhudi za kumtafuta huku Ubalozi ukiunda kikosi maalumu cha kufanya msako wa nyumba hadi nyumba ambapo baada ya kupita katika nyumba ya jirani alipokutwa marehemu katika shimo la maji machafu walipatwa na wasi wasi baada ya kuona kuna mabadiliko ya mbao zilizokuwa zimefunika shimo hilo.

Alisema awali walivyopita siku moja kabla waliona shimo hilo likiwa limefunikwa kwa mabanzi yaliyochakaa lakini siku ya pili yake asubuhi walikuta kukiwa na mabanzi mapya kuashiria kuna ukarabati umefanyika hali iliyowapa wasi wasi na kulazimika kulifunua shimo hilo na kumkuta marehemu akiwa amepoteza maisha ndani ya shimo  hilo.

Alisema aliyegundua kuwepo kwa mtoto ndani ya shimo ni ndugu yake alikuwa katika msako wa nyumba kwa nyumba na ndipo alipompigia simu akiwa kazini nayeye kutoa taarifa polisi na kwenye Serikali ya Mtaa ambapo walianza kufanya juhudi za kumtoa lakini walikwama hali iliyowalazimu kuomba msaada kwa kikosi cha Zimamoto na Uokoaji waliofanikiwa kumtoa majira ya saa Kumi jioni.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Nyibuko Pambogo kata ya Iyela Mage Makwenda alisema akiwa ofisini kwake alipokea taarifa za kupotea kwa mtoto katika mazingira ya kutatanisha lakini wakiwa katika juhudi za kumtafuta ndipo walioteuliwa kufanya upelelezi na msako mkali walipotoa taarifan za kuonekana kwa mtoto akiwa amefariki dunia ndani ya shimo la maji machafu.

Alimtaja mmiliki wa nyumba hiyo kuwa ni Gesho Kibonde (43) mkazi wa Mtaa wa Nyibuko kata ya Iyela Jijini hapa ambaye anashikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano pamoja na mkewe.

Kwa upande wake majirani na wakazi wa mtaa huo ambao hawakutaka majina yao kuandikwa walisema tukio hilo lina utata mkubwa kwa sababu baada ya mtoto kuonekana ndani ya shimo baadhi yao walifanikiwa kuchungulia na kumkuta marehemu akiwa amesimamishwa mithiri ya kutumbukiwa na mtu.

Mashuhuda hao waliendelea kusema kama mtotio angekuwa ametumbukia kwa bahati mbaya akiwa anacheza na wenzie angeonekana kuumia baadhi ya viungo lakini haikuwa hivyo pamoja na kuonekana kufa maji machafu ndani ya shimo hilo basi tumbo lake lingejaa lakini hali aliyokutwa nayo marehemu ni tofauti.

Hata hivyo wengine wamelihusisha tukio hilo na imani za kishirikina kwa madai kuwa aliyewaonesha kuwepo kwa mtoto ndani ya shimo hilo ni babu kutoka Mwakaleli( mganga)ambaye alifuatwa na baadhi ya watu ili kusudi awaoneshe mtoto na ndipo babu huyo alipo waambioa warudi katika nyumba ya jirani watamkuta akiwa hai.

Walisema baada ya kurudi na kutafuta katika eneo hilo waliokuta akiwa amekufa kitu ambacho waliamini ni kuchelewa kufika na kuligundua eneo lakini wanrwahi huenda wangemkuta marehemu akiwa mzima kabisa.

Aidha wakati zoezi la kumtoa marehemu ndani ya shimo hilo kwa ushirikiano wa Jeshi la Polisi, Zimamoto na Uokoaji pamoja na wafanyakazi wa Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira Mbeya( Mbeya uwsa) vilio vilitawala eneo hilo kutoka kwa wanawake walioshindwa kujizuia huku wengine wakipoteza fahamu na kulazimika kupewa msaada wa kupepewa.
Ikiwa kuna Gazeti litatumia habari hii tuwasiliane kwa namba 
0654221465
Na Mbeya yetu

No comments: