Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, September 12, 2013

SERIKALI YASHAURIWA KUZITEMBELEA ASASI ZA KIRAIA.

Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Women & Youth  Development Society, Sophia Mwakagenda, akiongea katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wajasiliamali wa mkoa wa Mbeya
Merina Mkuchu Afisa maendeleo ya biashara  SIDO mkoa waMbeya akifungua mafunzo hayo ya wajasiliamali wa mkoa wa Mbeya
Wajasiliamali wakiwa makini kujifunza
Mafunzo kwa vitendo


SERIKALI kupitia kitengo cha Ustawi wa Jamii imetakiwa kuzisimamia na kuzikagua baadhi ya Asasi ili kuzijua uhalali wake kutokana na kutokufanya kulingana na malengo ya usajili wake katika jamii.

Imeelezwa kuwa Asilimia kubwa ya Asasi  hizo zinafanya kazi ya kujiingizia kipato tofauti na hali halisi ya usajili wake ambao ni kuisadia jamii ili kuondokana na Umaskini na kuongeza vipato vyao.

Hayo yamebainishwa leo na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Women & Youth  Development Society, Sophia Mwakagenda, katika Mafunzo ya kuwajenga uwezo wa kuweka mali na kuongeza akiba kwa wajasiliamali wa Jiji la Mbeya, mafunzo yanayofanyika katika ukumbi wa Kiwira Motel.

Mwakagenda amesema baadhi ya Asasi hazifanyi kile kilichokusudiwa katika jamii hivyo ni Vema Serikali ikawa na utaratibu wa kuzikagua ili kujionea ufanisi wake na kama zinafanya kulingana na usajili wake na siyo kukaa na kusubiria ripoti maofisini.

Amesema katika mafunzo yanayoendelea katika ukumbi huo imeonekana kuwa na mwitikio mdogo uliotokana na baadhi ya Asasi kufanya mafunzo yasiyokuwa na tija kwa Mjasiliamali ambapo hufanya mafunzo kwa nia ya kujiingizia kipato na kuwaibia wananchi badala ya kuwaongezea kipato.

Amesema mafunzo hayo yatakuwa ya siku tatu ambayo yatawasaidia wananchi jinsi ya kuweka akiba na kuongeza mali kutokana na kubainika kuwa Wanawake wengi wanajiingiza katika mikopo ambayo huzidi kuwaletea umaskini hivyo kupitia mafunzo hayo wataweza kufundishwa namna ya kutumia fedha kwa nidhamu.

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa mafunzo hayo yanaendeshwa kwa ushirikiano wa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO), benki ya CRDB, Bacrays na Cokacola ambapo mbali na mafunzo hayo wajasiliamali hao watafundishwa pia namna ya utengenezaji wa bidhaa mbali mbali kama mishumaa, batiki na Sabuni mafunzo yatakayodumu kwa siku tatu kuanzia Septemba 12  hadi Septemba 14, Mwaka huu.




No comments: