Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, August 1, 2013

LIVE KUTOKA VIWANJA VYA NANENANE MBEYA MUDA HUU: UZINDUZI WA SIKUKUU YA WAKULIMA NANE NANE KANDA YA JUU KUSINI UNAENDELEA SASA VIWANJA VYA MWAKANGALE MBEYA


  Watu mbalimbali wakiwa katiaka viwanja vya Mwakangale Nane nane kwa ajili ya Kumsikiliza Mgeni Rasmi
 Ebony FM Radio wakiwa LIVE viwanja vya Nanenane
 Kikundi cha TOT Mbeya wakitumbuiza katika Shughuli za uzinduzi wa Nanenane Mbeya

 Mgeni Rasmi Waziri wa Uchukuzi Dr. Halison Mwakyembe Katikati akiwa meza kuu pamoja na viongozi mbalimbali
 Viongozi mbalimbali wakiwa katika Meza kuu
Katibu wa TASO Kanda ya nyanda za Juu Kusini Ramadhani Kiboko akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi
Waziri wa Uchukuzi ambaye alikuwa mgeni Rasmi Dr. Harison Mwakyembe akihutubuia.Waziri  wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ametoa miezi mitatu kwa matrekta  yote yanayobeba makontena  Bandarini kuondolewa na kupelekwa kwa wakulima mashambani kwa ajili ya shughuli za kilimo huku akisisitiza kwamba kazi hiyo siyo mahali pake.

Kauli hiyo ameitoa   leo kwenye ufunguzi wa maonyesho ya kilimo ya wakulima ya  nane nane ambayo kwa nyanda za juu kusini  yanayofanyika Jijini Mbeya  katika viwanja vya John Mwakangale Vilivyopo Uyole  ambapo  kauli mbiu yake ikiwa ni “Zalisha Mazao ya Kilimo na Mifugo kwa kulenga Mahitaji ya Soko”.

Amesema ifikapo Octoba 30 mwaka huu matrekta yote yawe yameshaondolewa ambapo pia atawasiliana na jeshi la Polisi   pamoja na Sumatra kuhakikisha wanasimamia zoezi hilo.

Amesema  Matrekta mengi ameyaona bandarini yakitumika kubeba mizigo, kwa mfano makontena, hivyo ameyataka matrekta hayo yanayotumika bandarini yaende yanakohitajika kwenye kilimo hivyo hataki s  kuyaona bandarini.

Amesema  Serikali imeweza kufuta ushuru wa zana za kilimo kama matrekta  chini ya kampeni ya Kilimo Kwanza,  lakini matrekta mengi yaliyoingizwanchini ili kuwezesha kilimo kukua yameishia kubeba mizigo bandarini kitu ambacho Serikali haiwezi kukubali kuona yanatumika kwa kazi hiyo.

Amesema uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo katika mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ipo chini ikilinganishwa na viwango vya utafiti, mfano hekta moja ya zao la mahindi inazalisha wastani wa tani tatu lakini utafiti unaonesha kwamba hekta moja ya zao la mahindi inaweza kuzalisha wastani wa tani saba za mahindi.

Aidha akizungumzia kwa upande wa maziwa wastani wa uzalishaji kwa ng’ombe mmoja kwa siku ni lita saba wakati kiwango kinachotakiwa kuzalishwa ni lita  20 kwa ng’ombe kwa siku.

Dk. Mwakyembe amesema upo umuhimu mkubwa wa kuyaongezea thamani mazao kwa njia ya viwanda vidogovidogo ili yauzike kwa haraka na kwa bei nzuri zaidi na kukidhi matakwa mbalimbali ya soko.
Ameongeza kuwa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini imetengewa zaidi ya Shs. 5 bilioni  kwa kazi ya kukarabati barabara vijijini, matumizi ya fedha hizo yakisimamiwa vizuri itasaidia kuleta  mabadiliko katika kusafirisha mazao vijijini.

Kuhusu sekta ya uchukuzi wa anga, reli na majini,alisema serikai inaendelea kuimarisha reli ya TAZARA kwa ushirikiano wa Serikali zetu mbili za Tanzania na Zambia, tuko kwenye maandalizi ya ujenzi wa reli kutoka Uyole kwenda Mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira, kuunganisha Tunduma na bandari ya Kasanga katika Ziwa Tanganyika.
***

Picha zote na Mbeya Yetu Blog


No comments: