Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, August 22, 2013

Hali si shwari TAZARA, Wafanyakazi, Walinzi na wastaafu waungana kudai kulipwa stahiki zao. Mbeya

Wafanyakazi wa Tazara wakijiandaa kwa maandamano kwend katika ofisi za mwajiri wao
Maandamano yameanza kuelekea kwa mwajiri
Akina mama wajana wakiwa katika ofisi za mwajiri Tazara kudai madai yao
Wastaafu wa tazara wakiwa wamekaa huku wakiwa na huzuni kubwa kwa kukosa mafao yao na kutopata majibu ya uhakika juu ya mafao yao
Juvenary Ngaiza  (mstaafu) na Aida Mbunda(Mjane) walisema tangu kustaafu kwao Serikali, Tazara na mashirika ya Pensheni yameshindwa kulipa stahiki zao kwa muda mrefu na wamekuwa hawatoi majibu ya kueleweka.
 Aida Mbunda(Mjane) 
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Tazara kanda ya Mbeya (TRAWU), Christopher Kazio, alisema hali ya wafanyakazi ni mbaya na inasababisha kuyumbisha usalama wa eneo husika kutokana na baadhi yao kufukuzwa katika nyumba walizopanga kutokana na ukosefu wa fedha.
Mwenyekiti wa wafanyakazi wa Tazara Mbeya Mjini Rafael Kazyoba, alisema Wafanyakazi wote kwa ujumla wamekubaliana kutofanya kazi yoyote hadi hapo uongozi wa Tazara utakapoamua kuwalipa mishahara yao na sio kutoa ahadi ambazo wameshindwa kuzitekeleza.
Baadhi ya watumishi wakiongea na waandishi wa habari
Ofisi ya mwajiri Tazara imefungwa lakini waandamanaji hao walisubiri hapohapo mpaka atakapotokea afisa huyo mwajiri ili awape jibu
Baadhi ya wafanyakazi wa Tazara wakiwa nje ya ofisi ya mwajiri



WAFANYAKAZI wa Shirika la Reli ya TAZARA Mkoani Mbeya wameingia katika Mgomo kwa muda usiojulikana wakishinikiza Uongozi wa Shirika hilo kuwalipa mishahara yao ya Miezi mine(4).

Aidha watumishi hao wapatao zaidi ya 400 pia wamemwomba Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuingilia mgogoro huo kwa kile walichodai kuwa Ahadi ya Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe aliyoitoa Agosti 3, Mwaka huu alipozungumza na wafanyakazi kuwa ameshindwa kuitekeleza.

Wakizungumza na waandishi wa Habari katika Ofisi za Tazara zilizopo Iyunga Jijini Mbeya baada ya Maandamano yaliyoishia katika Ofisi ya Mwajiri walisema Shirika hilo limeshindwa kuwalipa mishahara tangu Mwezi May Mwaka huu na kusababisha Wafanyakazi kuishi maisha ya tabu.

Walisema madai yao yameanza muda mrefu hali iliyopelekea Waziri Mwakyembe kufika na kuzungumza nao na kuahidi kuwa Ifikapo Agost 22, Mwaka huu Menejimenti iwe imelipa mishahara ya watumishi wote ikiwa ni pamoja na kukusanya madeni ya wateja wao yanayofikia Bilion 5.

Walisema hadi sasa hakuna kilichotekelezwa hali iliyowalazimu kugoma kujishughulisha na kazi yoyote inayohusu Tazara hadi hapo watakapolipwa Mishahara yao au Waziri Mkuu atakapoingilia na kutatua madai yao.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Tazara kanda ya Mbeya (TRAWU), Christopher Kazio, alisema hali ya wafanyakazi ni mbaya na inasababisha kuyumbisha usalama wa eneo husika kutokana na baadhi yao kufukuzwa katika nyumba walizopanga kutokana na ukosefu wa fedha.

Alisema hali ya usalama nayo si shwari kutokana na wafanyakazi kuanza kuiba baadhi ya vitu ili kujipatia chochote ili waweze kumudu ugumu wa maisha unaotokana na ukosefu wa fedha kwa zaidi ya miezi minne ambayo wafanyakazi wnalidai shirika.

Naye Mwenyekiti wa wafanyakazi wa Tazara Mbeya Mjini Rafael Kazyoba, alisema Wafanyakazi wote kwa ujumla wamekubaliana kutofanya kazi yoyote hadi hapo uongozi wa Tazara utakapoamua kuwalipa mishahara yao na sio kutoa ahadi ambazo wameshindwa kuzitekeleza.

Aidha kwa upande wa kampuni ya ulinzi inayolinda katika Stesheni ya Mbeya ya Kilumi Security nayo ikaibuka na kudai kuwa uongozi wa Tazara haujali maslahi ya watu na kutekeleza mikataba inayotakiwa na kwamba wao kama walinzi wanapata wakati mgumu wa kulinda usalama wa wafanyakazi walio na njaa wakiwemo wao wenyewe.

Jemsi Malembeka ni Afisa Rasilimali watu wa Kampuni hiyo ambaye alisema tangu waingie Mkataba wa kulinda maeneo ya Tazara takribani Miezi 6 imepita hawajawahi kulipwa hali inayosababisha walinzi kukimbia na wengine kujihusisha na wizi wa vitu vya Tazara.

Wakati madai ya wafanyakazi yakiendelea na huku wakitangaza mgomo mengine mapya yakaibuka baada ya Wazee wastaafu na wajane wa Tazara kukjitokeza na kudai kuwa tangu wastaafu kazi miaka ya 1993 Hadi 2003 hawajalipwa mafao yao.

Juvenary Ngaiza  (mstaafu) na Aida Mbunda(Mjane) walisema tangu kustaafu kwao Serikali, Tazara na mashirika ya Pensheni yameshindwa kulipa stahiki zao kwa muda mrefu na wamekuwa hawatoi majibu ya kueleweka.

Walisema ni vema mashirika hayo yakathamini mchango walioutoa wakiwa wafanyakazi wao na siyo kuwasahau baada ya kustaafu hali inayowapekea kunyanyaswa pindi wakianza kudai mafao yao ambayo ni haki yao.

Na Mbeya yetu


No comments: