Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, April 18, 2013

MICHEZO YA MEI MOSI KITAIFA YAZINDULIWA MBEYA


Mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa mbeya Ndugu   Costantine Mushi.
mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa mbeya Ndugu   Costantine Mushi. akizindua michuano hiyo



Michuano ya mei mosi kitaifa katika uwanja wa kumbukumbu sokoine jijini mbeya imeendela kushika ambapo hii leo michezo mbalimbali imefanyika uwanjani hapo  baada ya kufunguliwa rasmi na mwakilishi wa Mkuu wa mkoa wa mbeya Ndugu   Costantine Mushi.

Katika michezo ya awali kwa upande wa wanaume ilikuwa ni kati ya Wizara ya Mambo ya ndani pamoja na Wizara ya Mali asili.
Matokeo ya mchezo huo Timu ya Mambo ya Ndni imefanikiwa kuibuka kidedea kwa kuicharanga goli 3 kwa mbili timu pinzani.
Katika dk ya 22 maliasili walifanikiwa kuandika bao la kwanza kupitia kwa mchezaji wao Hamisi Changánda mara baada ya kupkea pasi kutoka wingi ya kulia.

 Katika kpindi hicho cha kwanza wapinzani wao ambao ni Mambo ya ndani walisawazisha bao hili katika dk 38 kwa mchezaji westoni mwanjala kwa kichwa ambapo mpaka mchezo huo unakamilika katika kipindi cha kwanza  timu zote zilikwenda suruhu.

Hata hivyo kipindi cha pili mpambano ulikuwa mkali kwani timu zote zilikuwa na kasi kubwa kwani dk ya .47 Andrew Bundara wa mambo ya nadani aliandikia timu yake bao la pili ambapo katika dk ya 60  Hamisi Nyagawa aliipachikia timu yake ya Maliasili bao la kusawazisha.

Mambo ya ndani waliendela kulindama lango la wapinzani wao na kufanikiwa kuandika bao la 3 na la ushindi kupitia kwa mchezaji wao hatari Westoni Mwanjala ambaye nfdite aliyekuwa kinara wa mapmbano huo kwa kuiandikia timu yake ya mambo ya ndani bao 3 katika kipindi chote cha dk 90 za mchezo.
Michezo mwingi ne wa pete kati ya CDA ya Dodoma pamoja Hazina Dar es salaam matokeo ni ,,,,,,,,,,,,CDA 31 Hazina 12…………Ulinzi ya Dar 38 Uhamiaji 17 .

Katika mchezo wa kuvuta kamba Hazina wanaume walishindwa nguvu na Uhamiaji.



2 comments:

Anonymous said...

Jamani, uwanja wa sokoine ufanyiwe ukarabati, unatia aibu jamani kwa jiji kubwa kama Mbeya. Wadau lioneni hilo

Anonymous said...

naomba picha zaidi na pia naomba toa taarifa za kila siku za michezo hadi siku ya kufunga nakutegemea wewe