Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, February 21, 2013

VIONGOZI na Watumishi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na vyama vya siasa vya upinzani ili kuwaletea maendeleo wananchi.



Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakati akifungua warsha juu ya Demokrasia na Stadi za uongozi inayotolewa kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Madiwani wa Mkoa wa Mbeya.

Mwaandaaji wa Mafunzo hayo Dk. Marry Mwanjelwa Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mbeya

Mfadhili wa Mafunzo hayo Dk. Stefan Chrobot ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa shirika la Fes- Tanzania kutoka Ujerumani 


Katibu wa CCM wilaya ya Mbeya mjini, Raymond Mwangwala,






VIONGOZI na Watumishi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano na vyama vya siasa vya upinzani ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk. Norman Sigalla ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakati akifungua warsha juu ya Demokrasia na Stadi za uongozi inayotolewa kwa viongozi wa Chama cha Mapinduzi pamoja na Madiwani wa Mkoa wa Mbeya.
  
Dk. Sigalla alisema Chama cha Mapinduzi ni mlango wa kuingilia ili kupata uongozi ili kuwahudumia wananchi lakini siyo sababu ya kuwachukia viongozi wa vyama vya upinzani.
  
" Si sahihi kugombana na na kiongozi wa chama kingine bali shirikianeni ili muwaletee maendeleo wananchi ambapo mtakapokuwa na ushirikiano na upendo ndipo watakapo watamani na kuhamia kwenye chama chenu" alisema Mkuu huyo.
  
Aliongeza kuwa Warsha zinazotolewa kwa viongozi zinasaidia kuwakumbusha wajibu wao kwa chama na kwa wananchi ili wasijisahau katika utendaji kazi wa kila siku ikiwa ni pamoja na kutekeleza Ilani za Chama.

Alisema kazi ya kiongozi wa Chama ni kujibu hoja za wananchi na siyo kiongozi kujifanyia mambo ambayo wananchi hawayahitaji na ambayo yanasababisha kuwachukia viongozi.
  
Kaimu Mkuu wa Mkoa huyo alisema ili Chama kiendelee kubaki madarakani ni wajibu wa Viongozi waliopewa dhamana na wananchi kuyatendea kazi madai yao ambayo yataepusha migogoro isiyokuwa na sababu.
  
Kwa upande wake Mwaandaaji wa Mafunzo hayo Dk. Marry Mwanjelwa Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Mbeya alisema mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya mkutano mkuu wa wajumbe wa CCM Taifa walioagizwa kuwajengea uwezoviongozi wa Chama.
  
Alisema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwakumbusha viongozi waliokuwepo madarakani kuhusu uwajibikaji pamoja na kuwajengea uwezo viongozi wapya walioingia madarakani hivi karibuni.
  
Naye mfadhili wa Mafunzo hayo Dk. Stefan Chrobot ambaye ni Mkurugenzi Mkazi wa shirika la Fes- Tanzania kutoka Ujerumani alisema wameamua kufadhili mafunzo hayo kutokana na shirika hilo kuwa na ushirikiano na Chama cha Mapinduzi.
  
Alisema kazi ya Shirika hilo ni kukuza demokrasia na utawala katika jamii, kuinua haki za binadamu za kupata huduma muhimu za kijamii na namna ya kuepukana na rushwa.


Na Mbeya yetu 

No comments: