Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, February 14, 2013

NMB WATOA MSAADA WA KOMPYUTA NA PRINTER KWA MBEYA SEKONDARI

Meneja mawasiliano wa NMB Josephine Kulwa akimkabidhi msaada wa kompyuta 2 na printer 1 Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Mbeya sekondari na pia ni mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na taka Mbeya  Eng. Simon Shauri hafla fupi hiyo ilifanyika shuleni hapo Mbeya sekondari
Mkuu wa shule ya Mbeya sekondari Mwamwitu Msigwa akimshukuru Josephine Kulwa kwa msaada waliopata toka NMB
Baadhi ya wanafunzi kwa niaba ya wenzao wakifurahia kupata kompyuta hizo
Walimu nao wa Mbeya sekondari hawakuwa nyuma kuja kupokea msaada huo  hapa wakiangalia kompyuta hizo
Baadhi ya watumishi wa NMB wakiwa makini kusikiliza shukrani zinazotolewa shuleni hapo
Meneja mawasiliano wa NMB Josephine Kulwa amewataka waalimu na wanafunzi hao kutumia vifaa hivyo kwa malengo yaliokusudiwa na kuvitunza ili na wengine wapate kuvitumia 
Mwenyekiti wa bodi ya shule ya Mbeya sekondari na pia ni mkurugenzi wa mamlaka ya maji safi na taka Mbeya  Eng. Simon Shauri akionyesha furaha yake wazi kwa wageni toka NMB kwa msaada waliotoa kwa shule yao na ameahidi kuwa kompyuta hizo zitatumika kwa malengo yaliokusudiwa 
Mkuu wa shule ya Mbeya sekondari Mwamwitu Msigwa pia nae amewashukuru sana NMB kwa msaada waliotoa kwa shule yake
Huu ndiyo msaada wa kompyuta na printer toka NMB

Picha na Mbeya yetu

No comments: