Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, January 23, 2013

Tuhuma za rushwa ya uchaguzi wa ndani kuwaondoa baadhi ya viongozi wa UVCCM na CCM Mbeya

 KATI KATI NI MWENYEKITI WA ccm ALIYEMALIZA MUDA WAKE 2012 WILAYA YA MBEYA VIJIJINI WILLIUM SIMWALI

BAADHI ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na baadhi ya jumuiya zake ikiwemo ile ya vijana (UVCCM) mkoani Mbeya wanatarajiwa kuhamishwa na uchaguzi kurudiwa baada ya kubainika na kulalamikiwa kujiingiza katika vitendo vya kuomba, kupokea na kutoa rushwa.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho, zimeeleza kuwa baada ya uchaguzi huo baadhi ya wanachama walipeleka malalamiko ngazi za juu za chama na utafiti ukawa unaendelea.

Imeelezwa kuwa waliolalamikiwa na kuhojiwa ni pamoja na makatibu wa chama hicho ngazi za wilaya na baadhi ya wagombea wa nafasi mbalimbali na baadhi wameshindwa kujieleza.

Mmoja wa kiongozi wa UVCCM, anadaiwa kutumia cheti cha ubatizo ambacho hakiendani na jina lake hali ambayo inatafsiriwa kuwa alipita na kuchaguliwa isivyo halali na kwamba kuna wengine ambao wanajihusisha na uimarishaji wa makundi ya wanaohitaji kugombea nafasi ya Rais mwaka 2015.

Katibu wa CCM katika wilaya ya Mbeya Vijijini ni mmoja wa makatibu ambao wanatajwa kuwa anaweza kuhamishwa kutokana na malalamiko kadhaa ya wanachama wa wilaya hiyo.

Hata hivyo, uchunguzi uliofanywa na mtandao huu, umebaini kuwa baadhi ya waliotangazwa kushinda katika nafasi kadhaa za chama hicho katika wilaya hiyo ni batili kwasababu wagombea ambao kura zilitosha hawakuweza kutangazwa kutokana na kutoweza kuchangia fedha zilizodaiwa kuwa ni za maandalizi ya uchaguzi


 HABARI KWA HISANI YA PASTOR GORDON KALULUNGA

No comments: