Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, December 8, 2012

MTOTO WA MIAKA SABA AACHIWA MTOTO MCHANGA NA MWANAMKE ASIYEJULIKANA MBEYA

Mtoto Sharifu huyoo wa darasa la pili shule ya msingi Mbata akiletwa na wenzake kuja kuzungumza na waandishi wa habari waliokwenda kumtembelea shuleni hapo ili kujua kisa kilichomtokea mpaka akaachiwa mtoto
Kazi kweli kweli  watoto wakimwimbia wimbo wa kumtania sharifu kuwa kapakaziwa mtoto
Kwakweli tulikuta watoto wa shule ya msingi Mbata wamechangamka sana na kutupokea vizuri
Sharifu huyo katikati jamani  sasa mwachieni  tunashukuru kwa kutuletea tuongee nae
Rafiki yetu sharifu tayari wenzake wamemwachia na anaanza kutupa kisa cha kuachiwa mtoto mchanga

Sharifu 7 amesema yeye alipokua anatoka shule mida ya saa nne asubuhi kuna mama alimwita huyo mama alikuwa amebeba mtoto mchanga na ndipo mama huyo akamwambia sharifu naomba nisaidie kumbeba mtoto kwani nimesahau kuchukua kitu fulani nyumbani 

sharifu bila kujua akamchukua mtoto huyo  na mama wa mtoto akaondoka  sharifu anasema ilipita muda mrefu sana bila ya kumuona tena mama huyo na mtoto huyo alianza kulia na sharifu kuona mtoto analia nayeye akaanza kulia
Ndipo akatokea mwanafunzi huyu na kumuuliza sharifu mbona unalia na mtoto analia? sharifu akamjibu mwanafuzi mwenzake kuwa kuna mama kaniachia mtoto toka saa nne mpaka sasa sijamwona mama huyo nae nami nimechoka kumbeba ndipo mwanafunzi huyo akamwambia twende tumpeleke kwa walimu
Upendo Mwakipunda mwalimu wa shule ya msingi mbata amekiri kutokea kwa tukio hilo kweli walimpokea mtoto huyo na kumpeleka kituo cha polisi 
Tukiwa na mtoto sharifu baada ya kuongeanae habari kamili ya tukio hili tutawaletea jumatatu mara baada ya kufuatilia polisi na hospitali ya rufaa Mbeya
Kwa ujumla baada ya kumaliza maongezi tulianza kuona jinsi watoto wakiwa katika michezo mbalimbali shuleni hapo dogo katulia dirishani mwa darasa lake huku akipata embe kwa raha zake

Wengine madirishani wengine wanachora ukuta ni furaha tu shuleni hapo

Wa kuruka kamba haya wa kucheza mpira sawa
Wanafunzi wakifurahia chandarua walichobuni shuleni hapo

Wakifurahia kutembelewa shuleni kwao
Picha na mbeya yetu

No comments: