Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, August 29, 2012

KUKOSEKANA KWA OFISI ZA SHIRIKA LA VIWANGO (TBS) MBEYA VIWANDA VIDOGODOGO VYA KUSINDIKA CHAKULA NA MAFUTA YA KULA HAVIJAWAHI KUKAGULIWA WALA KUJUWA UBORA WAKE KWA WALAJI

Muuza mafuta ya alizeti maeneo ya soko la sido Mwanjelwa Mbeya akiendelea kujaza mafuta ya alizeti kwenye mageroni ya lita tano na moja toka mojakwamoja kwenye kiwanda bila ya kukaguliwa wala kujua ubora wake kwa mlaji 
Mama huyu kamera yetu ilimnasa akizoa mabaki ya mafuta toka kwenye mapipa  kiwandani hapo
Hii ndiyo hali halisi ya viwanda vyakukamulia mafuta ya alizeti jijini Mbeya tunaimani wahusika wa afya mpo na mnaliona hili
Mama huyu muuza mafuta ya alizeti akitoa karatasi ya nembo ya maji ya rungwe ili mlaji asijue kuwa chupa hiyo ilitumika kuhifadhia maji je usafi wa kusafisha chupa hizo husimamiwa na nani? maana chupa nyingi huokotwa mitaani na majalalani
Mama Asha moja ya wamiliki wa mashine za kukamua mafuta aina ya alizeti Mbeya yetu ilipomuuliza je ameshawahi kukaguliwa ubora wa mafuta anayokamua kwenye kiwanda chake  amesema hajawahi tangu aanze biasharayake hiyo zaidi ya miezi sita iliyopita 
Hii bidhaa baadhi ya kina mama wameilalamkia haina ubora na inawatoa vidonda hatujapenda kutoa picha za akina mama hao walioleta ila zipo na kila mhusika tukimuuliza anasema watu wa viwango ndiyo wanahusika sasa mbeya hakuna ofisi za viwango je wafanyeje akina mama hao waliopata matatizo?
Afisa mamlaka ya chakula na dawa mbeya tulipomuuliza juu ya swala hili la hifadhi ya  wanawake yaani always alisema ofisi yake haiusiki na kukagua bidhaa hizo badalayake akatueleza tuende ofisi za TBS yaani shirika la viwango  ambalo nalo Mbeya hawana ofisi wala mwakilishi yaani sasa tumebaki hewani na kujiuliza sasa nani muhusika?

No comments: