Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Sunday, April 22, 2012

LOWASSA ACHANGIA MILIONI 10 KANISA LA EAGT TUNDUMA MBEYA

Bw. Lowassa ambaye alikuwa akikimbizana na muda aliamua kuondoa udhia kwa kusimama moja kwa moja jukwaani wakati baadhi ya waumini wakitoa ahadi za kuchangia fedha za ujenzi wa kanisa hilo na kusema kuwa anawaomba radhi waumini wa kanisa hilo na kisha akatoa kitita cha fedha zilizofungwa na bahasha ya kaki na kumkabidhi Askofu wa kanisa hilo Keneth Kasunga.




Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Edward Ngoyai Lowassa ametoa shilingi milioni 10, kwa ajili ya ujenzi wa Kanisa la EAGT lililopo Mji mdogo wa Tunduma, Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya.

Fedha hizo zimetolewa jana katika harambee ya kuchangia ujenzi wa Kanisa hilo, iliyofanyika katika viwanja vya Hoteli ya High Class mjini humo.

Lowasa alitumia zaidi ya dakika 28 pekee kuwepo kwenye viwanja hivyo ambapo amesema kuwa watanazania wanapaswa kuwa na wito wa kujenga nyumba za kuabudu kuliko kujenga zaidi nyumba za starehe zikiwemo Bar.

Amesema kuwa amefurahi kualikwa katika harambee hiyo na kwamba kwa sasa nchi ipo kwenye kipindi kigumu cha uchumi na masuala ya katiba mpya, hivyo amewaomba wakristo kupanga ratiba ya kuiombea nchi ili iendelee kuwa na amani na watanzania kuendelea kuimarisha ushirikiano na umoja wa kitaifa uliopo nchini.

Aidha, amesema jambo hilo ni muhimu kwa kila mtanzania akiliombea taifa, Tanzania haitaweza kutokea migogoro na vita za wenyewe kwa wenyewe kama ilivyo kwa mataifa mengine mfano Nigeria.

Baada ya hotuba yake hiyo fupi aliwaita wasaidizi wake jukwaani na kuwaagiza wampande na mfuko wa fedha na kisha akamkabidhi mfuko wa pesa taslimu shilingiu milioni 10, Askofu Keneth Kasanga wa kanisa hilo.

Kwa uapnde wake Askofu huyo alimshukuru Waziri mstaafu Lowasa ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Monduli kuwa amejenga nyumba ya Mungu na hawezi kumuacha katika mambo yake yote na mahitaji pia.

Kanisa hilo lina zaidi ya waumini 750, walipanga kuwa na kiasi cha shilingi milioni 750 na siku hiyo zimekusanywa jumla ya shilingi milioni 17.9, huku fedha zilizoahidiwa ni shilingi milioni 

Habari kwa hisani ya kamanga na Rashidi Mkwinda

No comments: