Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, February 10, 2012

MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA MBEYA AGOMEWA NA WAFANYABIASHARA WA SOKO LA SOWETO MBEYA KUWA HAWATALIPA USHURU MPYA MPAKA MIUNDO MBINU YA SOKO HILO IBORESHWE

Mstahiki meya wa jiji la Mbeya Athanas Kapunga akiongea na wafanyabiashara wa soko la soweto jijini mbeya apata wakati mgumu kujibu maswali ya wafayabiasha hao
Wafanyabiashara hao wa soko la soweto wakimsikiliza meya wa jiji la mbeya
Wafanyabiashara wa soko la soweto wakionyesha vidole viwili juu kuwa watalipa sh 200 tu na  si sh 300 iliyotangazwa na halamshauri ya jiji la mbeya wamedai kuwa endapo halmashauri inataka walipe sh 300 basi waboreshe miundo mbinu ya  soko hilo kwani ni chafu na barabara zake hazipitiki kipindi hiki cha mvua
Mstahiki meya wa jiji la mbeya akiongozana na wananchi kwenda kukagua soko hilo la soweto
Hii ndiyo hali halisi ya barabara za soko hilo meya wa jiji akiendelea kukagua soko
Hii ndiyo barabara ya kuingia soko hilo la soweto jijini mbeya
Meya wa jiji la mbeya akionyeshwa mfereji wa maji machafu uliopo katikati ya soko hilo la soweto
Shimo la maji taka lipo katikati ya soko huku likitiririsha maji machafu na pembeni ya ke ni baadhi ya magunia ya matunda mbalimbali
Mara baada ya kutembelea soko hilo mstahiki meya amemuagiza mkurugenzi wa jiji la mbeya kuwa kuanzia leo muanze kumwaga kifusi cha kutengenezea barabara na kukarabati miundo mbinu yote ya soko

No comments: