Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, October 21, 2011

WAOMBA MSAADA WA FEDHA ILI KUFANIKISHA ZOEZI LA UFUNGAJI WA MITAMBO YA UMEME NUNGU - MAKETE

Wananchi wa kijiji cha Nungu wilaya ya Makete mkoani Iringa wameiomba serikali iweze kuwasaidia kiasi cha fedha ili waweze kufanikisha zoezi la ufungaji wa mitambo ya umeme katika maporomoko ya mto Mbulu.

Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho Bwana Esau Ndaga amesema ili kufanikisha zoezi la ufungaji wa mitambo hiyo msaada mkubwa unahitaji kutoka Serikalini na wadau wengine wa maendeleo.

Naye mwenyekiti wa kijiji hicho Bi.Marieth Malekano amesema wamefanikiwa kumpata mkandarasi wa kufunga mitambo hiyo ambapo gharama inayohitajika ni shilingi milioni 20.

No comments: