Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, October 22, 2011

WANANCHI WA JIMBO LA RUNGWE MASHARIKI WAFANYA IBADA YA MAOMBI KUMWOMBEA WAZIRI PROF MWANDOSYA APONE MAPEMA


Prof Mark Mwandosya ambaye ni Waziri wa maji na Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki.
*****
Na mwandishi wetu
Wananchi wa Jimbo la Rungwe Mashariki wamefanya ibada maalum ya kumwombea Mbunge wa Jimbo hilo ambaye pia ni  Waziri wa maji Profesa. Mark Mwandosya ili apone haraka.

Baada ya ibada hiyo maalumu mmoja wa wakazi wa jimbo hilo Njwaba Mwakambinda amesema wananchi wa Kijiji hicho wanafarijika wanaposikia taarifa njema kuhusu hali ya afya ya Mbunge wao.

Naye mwenyekiti wa wataalamu mkoa wa Mbeya Prince Mwaihojo amesema kuwa wananchi wanatakiwa kuondoa itikadi zao za kisiasa katika kuleta maendeleo katika Jimbo hilo na kuombeana mema badala ya kutumia siasa kuzushiana vifo.

Akijibu baadhi ya masuala yaliyojitokeza eneo hilo, Msaidizi wa Prof. Mark Mwandosya, Ndigwako Mwasandungila ambaye pia ni diwani wa kata ya Lwangwa amesema mbunge wao anaendelea vizuri na anaendelea kutekeleza kwa vitendo ahadi zake akiwa kwenye matibabu

No comments: