Na blogu ya Francis Godwin
WAKATI vyama vya siasa katika wilaya ya Iringa mjini vikiendelea kukamiana katika kampeni za lala salama kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa diwani wa kata Gangilonga na Kitanzini katika jimbo la Iringa mjini hapo jumapili wiki hii chama cha NCCR- Mageuzi kimelazimika kusimamisha kampeni zake kwa muda usiojulikana kutokana na kifo cha ghafla cha wakili maarufu wa kujitegemea mkoa wa Iringa Nelson Thomas Mwakingwe (pichani) ambaye pia alikuwa ni mme mwekahazina wa Taifa wa chama hicho Mariam Mwakingwe.
Huku chama cha mapinduzi (CCM) na chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) vikituma salam za rambirambi pamoja na kuungana na NCCR-Mageuzi katika kusitisha kampeni kwa muda.
Mwenyekiti wa NCCR - Mageuzi wilaya ya Iringa mjini Nasra Mwampeta ambaye pia ni mgombea udiwani wa kata ya Kitanzini alimweleza mwandishi wa habari hizi jana kuwa chama chake kimelazimika kusitisha kampeni hizo kutokana na msiba huo mkubwa kwa wakazi wa mji wa Iringa.
Alisema kuwa kifo cha ghafla cha wakili huyo kimewashitua wakazi wa mji wa Iringa hivyo NCCR- Mageuzi kutokana na msiba huo kimelazimika kusimamisha shughuli zote za kampeni katika kata ya Gangilonga na Kitanzini ili kupisha maombolezo kwa wananchi wa mji wa Iringa.
Mwampeta ambaye pia ni mgombea wa kata ya Kitanzini aliwaomba radhi wananchi wa kata hiyo ya kitanzini kwa kutoendelea kupata sera za NCCR-Mageuzi kabla ya uchaguzi mkuu japo aliomba siku ya kupiga kura kuchagua chama hicho kwa kata ya Gangilonga kumpigia kura Karimu Masasi (NCCR-Mageuzi).
Mbali ya kuwa wakili Mwakingwe pia alipata kuwa diwani wa kata ya Gangilonga kupitia NCCR-Mageuzi kati ya mwaka 1995 hadi 2000.
Kwa upande wake katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa mjini Lusiana Mbosa alisema kifo cha wakili Mwakingwe ni pigo kubwa kwa wananchi wa manispaa ya Iringa bila kujali itikadi zao za vyama kwani marehemu enzi za uhai wake alikuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika masuala ya sheria.
Mbosaa alisema kuwa CCM kwa siku ya jana ililazimika kusitisha shughuli za kampeni kwa ajili ya kuungana na wafiwa katika kuomboleza msiba huo mzito na kuwa katika kata ya Gangilonga CCM pia imepata kusimamisha mgombea wake Nicolina Lulandala huku Kitanzini ikimsimamisha Jasca Msambatavangu.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wilaya ya Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa mbali ya kutoa pole kwa wafiwa bado alisema kuwa Chadema Iringa imepokea kwa masikitiko kifo cha wakili huyo na kuwa itaungana na wafiwa na wakazi wa mji wa Iringa siku ya jumamosi katika mazishi.
Msigwa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Iringa mjini alisema kuwa Chadema imemsimamisha Edwin Sambala kwa kata ya Gangilonga na Kitanzini Gervas kalolo na kuomba wananchi kutumia haki yao kuchagua viongozi wa Chadema bila kutishwa na mtu.
Wakili Mwakingwe alifariki ghafla dunia usiku wa kuamkia jana akiwa katika hospital ya mkoa wa Iringa kabla ya kifo chake Mwakingwe alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kisukari
WAKATI vyama vya siasa katika wilaya ya Iringa mjini vikiendelea kukamiana katika kampeni za lala salama kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa diwani wa kata Gangilonga na Kitanzini katika jimbo la Iringa mjini hapo jumapili wiki hii chama cha NCCR- Mageuzi kimelazimika kusimamisha kampeni zake kwa muda usiojulikana kutokana na kifo cha ghafla cha wakili maarufu wa kujitegemea mkoa wa Iringa Nelson Thomas Mwakingwe (pichani) ambaye pia alikuwa ni mme mwekahazina wa Taifa wa chama hicho Mariam Mwakingwe.
Huku chama cha mapinduzi (CCM) na chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) vikituma salam za rambirambi pamoja na kuungana na NCCR-Mageuzi katika kusitisha kampeni kwa muda.
Mwenyekiti wa NCCR - Mageuzi wilaya ya Iringa mjini Nasra Mwampeta ambaye pia ni mgombea udiwani wa kata ya Kitanzini alimweleza mwandishi wa habari hizi jana kuwa chama chake kimelazimika kusitisha kampeni hizo kutokana na msiba huo mkubwa kwa wakazi wa mji wa Iringa.
Alisema kuwa kifo cha ghafla cha wakili huyo kimewashitua wakazi wa mji wa Iringa hivyo NCCR- Mageuzi kutokana na msiba huo kimelazimika kusimamisha shughuli zote za kampeni katika kata ya Gangilonga na Kitanzini ili kupisha maombolezo kwa wananchi wa mji wa Iringa.
Mwampeta ambaye pia ni mgombea wa kata ya Kitanzini aliwaomba radhi wananchi wa kata hiyo ya kitanzini kwa kutoendelea kupata sera za NCCR-Mageuzi kabla ya uchaguzi mkuu japo aliomba siku ya kupiga kura kuchagua chama hicho kwa kata ya Gangilonga kumpigia kura Karimu Masasi (NCCR-Mageuzi).
Mbali ya kuwa wakili Mwakingwe pia alipata kuwa diwani wa kata ya Gangilonga kupitia NCCR-Mageuzi kati ya mwaka 1995 hadi 2000.
Kwa upande wake katibu wa chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Iringa mjini Lusiana Mbosa alisema kifo cha wakili Mwakingwe ni pigo kubwa kwa wananchi wa manispaa ya Iringa bila kujali itikadi zao za vyama kwani marehemu enzi za uhai wake alikuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika masuala ya sheria.
Mbosaa alisema kuwa CCM kwa siku ya jana ililazimika kusitisha shughuli za kampeni kwa ajili ya kuungana na wafiwa katika kuomboleza msiba huo mzito na kuwa katika kata ya Gangilonga CCM pia imepata kusimamisha mgombea wake Nicolina Lulandala huku Kitanzini ikimsimamisha Jasca Msambatavangu.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wilaya ya Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa mbali ya kutoa pole kwa wafiwa bado alisema kuwa Chadema Iringa imepokea kwa masikitiko kifo cha wakili huyo na kuwa itaungana na wafiwa na wakazi wa mji wa Iringa siku ya jumamosi katika mazishi.
Msigwa ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Iringa mjini alisema kuwa Chadema imemsimamisha Edwin Sambala kwa kata ya Gangilonga na Kitanzini Gervas kalolo na kuomba wananchi kutumia haki yao kuchagua viongozi wa Chadema bila kutishwa na mtu.
Wakili Mwakingwe alifariki ghafla dunia usiku wa kuamkia jana akiwa katika hospital ya mkoa wa Iringa kabla ya kifo chake Mwakingwe alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kisukari
Wakili Mwakingwe atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa aliopata kuutoa katika jamii ya wakazi wa mkoa wa Iringa ikiwa ni pamoja na kusaidia wanyonge kupata haki zao kwa kuwatetea akiwa kama wakili .
Pia alikuwwa ni mmoja kati ya mawakili waliopenda kujichanganya na jamii zaidi na kuwa jirani na wananchi na ni wakili pekee aliyepata kuingia katika ulingo wa siasa.
Kifo cha wakili Mwakingwe si pigo tu kwa familia bali ni pigo kwa Taifa zima kutokana na kupunguza idadi ya mawakili wa kujitegemea hapa nchini na kifo hiki ni pigo kwa chama cha NCCR Mageuzi kutokana na marehemu alipata kuwa diwani wa chama hicho japo kwa upande mwingine kifo cha wakili Mwakingwe kinakwamisha kampeni za uchaguzi mdogo kwa kata ya Gangilonga na Kitanzini kwa chama cha NCCR Mageuzi kutokana na mke wa Marehemu Bi Mariam kuwa ni mratibu mkuu wa kampeni hizo na ndiye nguzo ya NCCR kwa mkoa wa Iringa.
Kifo chake kimepokelewa kwa majonzi makuwa na wakazi wa mji wa Iringa ambao kwa nyakati tofauti wamepata kueleza masikitiko yao.
Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi wa CCM Iringa mjini Eliud Mvella Wamahanji anasema kuwa marehemu alikuwa ni shemeji yake na kuwa amepata taarifa ya msiba huo akiwa safarini kurejea Iringa na kuwa kifo hicho ni pigo kubwa ndani ya familia .
Deus Kalinga ni mkazi wa Gangilonga anasema kuwa kwa upande wake bado haamini kama kweli wakili huyo amefariki dunia na kueleza kuwa Mwakingwe ni mmoja kati ya mawakili waliokuwa wazalendo na kusaidia watu wenye shida.
No comments:
Post a Comment