Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, December 3, 2015

WAHITIMU WA CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA(CBE) KAMPASI YA MBEYA WAPATIWA MAFUNZO YA UJASILIAMALI.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Taaluma, Profesa Saimon Msanjila akifungua semina ya siku mbili ya ujasiliamali kwa Wahitimu wa CBE Kampasi ya Mbeya(hawapo pichani)

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma CBE miaka ya nyuma(ALUMNI) Boyd Mwakyusa akimkaribisha mgeni rasmi kufungua mafunzo ya ujasiliamali kwa wahitimu wa chuo cha CBE Kampasi ya Mbeya.

Katibu wa ALUMNI ambaye pia ni mkufunzi wa Ujasiliamali, Graciano Kunzugala, akitoa utambulisho kwa wageni na wanafunzi waliohudhuria mafunzo ya ujasiliamali

Baadhi ya Watumishi wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Kampasi ya Mbeya wakijiandaa kupokea wageni kwa ajili ya mafunzo ya ujasiliamali katika ukumbi wa Hoteli ya Mount Livingstone

Kunzugala akiendelea kutoa mafunzo kwa wahitimu





Wahitimu wakifuatilia kwa makini semina inayotolewa




WAHITIMU wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)Kampasi ya Mbeya wamepatiwa mafunzo ya ujasiliamali ili kujiandaa na soko la ajira pindi watakaporudi uraiani.

Wahitimu hao wamepatiwa mafunzo ya siku mbili yanayofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Mount livingstone iliyopo jijini Mbeya mafunzo yaliyoandaliwa na Umoja wa Wanafunzi waliowahi kusoma CBE miaka ya Nyuma Kanda ya Nyanda za juu kusini( ALUMNI).

Akizungumza katika ufunguzi wa Semina hiyo iliyofunguliwa na Makamu Mkuu wa Chuo cha CBE Taaluma, Profesa Saimon Msanjila, Mwenyekiti wa ALUMNI Kanda ya Nyanda za juu kusini, Boyd Mwakyusa amesema lengo la mafunzo ni kuwaandaa wahitimu kujiajiri wenyewe.

Alisema mafunzo ya siku mbili pia yatahudhuriwa na baadhi ya watu mashuhuri ambao walisoma CBE miaka ya nyuma na kupata mafanikio ili waweze kutoa changamoto na njia zilizowasaidia kupata mafanikio.

Awali akifungua mafunzo hayo, Profesa Msanjila alisema majukumu ya wahitimu ni kukisaidia Chuo kwa kukitangaza na kufanya mambo mazuri kwenye kazi na jamii jambo ambalo litasaidia kuleta sifa nzuri ya Chuo na hatimaye kuongeza idadi kubwa ya wanafunzi.

Msanjila alisema Wahitimu wanapaswa kwenda kuwa mabalozi wa Chuo kila mahali watakapokuwepo ambapo hivi sasa Chuo kimeshinda kuwa Chuo chenye mabadiliko Chanya kwa mwaka 2015  na kuzawadiwa cheti.

“Mnapoenda huko mkafanye kazi vizuri pia mnayonafasi ya kujiuliza namna mlivyopokelewa chuoni wakati mnaanza pia mjitafakari namna mtakavyoendelea kutoa michango yenu kwa uongozi wa Chuo” alisema Makamu Mkuu wa Chuo.

Kwa upande wake Katibu wa ALUMNI, Graciano Kunzugala ambaye pia ni mkufunzi wa ujasiliamali alisema Mkioa ya nyanda za Juu kusini inakabiliwa na tatizo la Biashara kwani asilimia kubwa hufanya biashara ya kubangaiza na kuigana.

Alisema mfanyabiashara wa kweli ni mjasiliamali kwani anafanya biashara yenye malengo ya muda mfupi, kati na muda mrefu pia anakuwa na mikakati inayolenga kukuza biashara yake yenye mwelekeo wa kukuza uchumi.




No comments: