Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, October 19, 2015

MAKONDA AWASHUKIA WAMILIKI WA MAGARI

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akizungumza katika mkutano na madereva wa magari makubwa Mpemba wilayani Momba.

Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva Shaban Mdem akitoa taarifa fupi kuhusu maendeleo ya madai ya mareva kutoka serikalini na Wamiliki.

Naibu Katibu Mkuu na Msemaji wa Umoja wa Madereva, Rashid Saleh akizungumza katika kikao cha Madereva


Baadhi ya madereva waliojitokeza katika mkutano uliofanyika Mpemba Wilaya ya Momba Mkoani Mbeya.


WAMILIKI wa Magari ya usafirishaji wametakiwa kutowapangia madereva wao juu ya kumchagua mgombea Fulani katika uchaguzi mkuu kwa ajili ya maslahi yao binafsi.
 
Aidha wamepaswa kuwaachia wao wenyewe kumchagua kiongozi ambaye wanaona ana sera nzuri na zenye kumgusa mhusika moja kwa moja na sio kwa shinikizo lenye kuendelea kumkandamiza dereva.
 
Wito huo ulitolewa na Mlezi wa Umoja wa Madereva Tanzania(TADWU), Paul Makonda ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni alipokuwa akizungumza nao katika mkutano wao uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Uwanji iliyopo Mpemba wilayani hapa Mkoa wa Mbeya.
 
Makonda alisema zipo dalili za wamiliki wa magari kuwapangia madereva mtu wa kumpigia kura katika uchaguzi ujao jambo ambalo linaondoa demokrasia na uhuru wa Mtanzania kumchagua kiongozi anayemtaka na anayeona anafaa kuwaletea maendeleo.
 
“Zipo taarifa kuwa wamiliki wanawashinikiza kumchagua kiongozi Fulani hili sio jambo zuri pimeni wenyewe ni nani anagusa maslahi yenu na yupi akiingia ikulu atawasaidia moja kwa moja hao wamiliki wanawashinikiza mmchague wanaemtaka ili waendelee kuwakandamiza hivyo kuweni makini” alisisitiza Makonda.
 
Aliongeza kwa kuwahimiza madereva hao kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili kumchagua kiongozi bora na kwamba wasimchague ambaye anatoa ahadi ya kuongeza boda boda ili hali wao wanaendesha magari.
 
“Hakikisheni siku ya uchaguzi mnajitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura ila usitake kumchagua kiongozi kwa ahadi ya boda boda wakati wewe unaendesha Roli itakusaidiaje” alisema Mlezi huyo.
 
Makonda alisema uchaguzi wa mwaka huu ni muhimu kwa sababu umejaa historia na ni uchaguzi wa kimapinduzi kwani inaonesha kila awamu kuwa na mabadiliko tangu awamu ya kwanza hadi awamu ya nne hivyo awamu ya tano inapaswa kufuata mtililiko huo.
 
Alisema awamu ya kwanza Mwalimu Nyerere alikuwa mkali lakini alipombadili Rais Mwinyi katika awamu ya pili alikuwa mpole ndipo alipoingia Benjamini Mkapa katika awamu ya tatu akiwa mkali na sasa Rais anayemalizia muda wake Jakaya Kikwete ni Mpole hivyo anapaswa kufuatwa na Rais wa awamo ya tano ambaye ni mkali.
 
Awali Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva(TADWU), Shaban Mdem, alimpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa jinsi alivyojitoa kupigania maslahi yao na hatimaye kufikia katika hatua nzuri kati ya Serikali, Wamiliki na Madereva.
 
Alisema kwa muda mfupi wamefanikiwa kusajili Chama cha wafanyakazi ambacho katika umoja huo wameweza kukutana na Rais ili kuzungumzia changamoto walizikuwa nazo ambazo zilizpelekea kuwepo kwa migomo na hatimaye kufikia katika hatua nzuri.
 
Alisema mambo ambayo wameshakubalina bado hatua za mwisho ni kuhusiana na posho ambapo kila dereva atapaswa kulipwa shilingi 70,000 kwa siku kutoka Dar es salaam hadi Tunduma pamoja na fedha ya safari shilingi 35,000 na kwamba baada ya kuvuka geti Dereva atalipwa dola 75 kwa siku.
 
Akizungumzia suala la wamiliki kuwataka kumchagua kiongozi wanayemtaka wao Mwenyekiti huyo alisema jambo hilo lipo na tayari madereva zaidi ya 40 walibainika kusambaza ujumbe mfupi wenye kumpigia debe kiongozi wanaemtaka wamiliki.
 
Alisema hata hivyo madereva hao walionywa kutoendelea na hatua hiyo na kusubiri tamko la madereva kwa pamoja juu ya kiongozi anayepaswa kupigiwa kura tofauti na shinikizo la wamiliki.
 


No comments: