Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, May 9, 2015

WAKAZI WA TUNDUMA WAMETAKIWA KUUTUNZA MJI WAO

 Mwenyekiti wa Umoja wa vijana UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna akiwa meza kuu wakipiga makofi pamoja na viongozi wengine.
 Katibu Wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Mbeya, Bi Khadija akiwasalimia wananchi wa Kata ya Sogea katika mji mdogo wa Tunduma.
 Mwenyekiti wa Umoja wa vijana UVCCM Mkoa wa Mbeya Amani Kajuna akihutubia wananchi wa Tunduma kwenye mkutano wa hadhara.
 Awilo kidume cha Mbeya akitoa burudani.
 Makhirikhiri wakitumbuiza.
 Wakazi wa Tunduma wakisikiliza kwa makini.
Wakazi na wanachama wa ccm wakifuatilia kwa makini na kushangilia katika mkutano wa hadhara.

WAKAZI wa Mji mdogo wa Tunduma wilayani Momba Mkoa wa Mbeya wametakiwa kuutunza mji huo kama kitovu cha biashara kwa Mkoa wa Mbeya na mpaka unaotegemewa  na nchi jirani.

Wito huo ulitolewa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa wa Mbeya, Amani Kajuna alipokuwa akihutubia vijana na wananchi wa Mji wa Tunduma katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa na Kata ya Sogea.

Kajuna alisema Wakazi wa Tunduma wamekuwa wakikubali kutumika katika vurugu za kisiasa na kufanya maandamano ambayo yanapelekea kuvunjika kwa amani katika mji huo na kusababisha kuyumba kwa uchumi na mzunguko wa kibiashara kwa ujumla kwa Mkoa wa Mbeya na Taifa kwa jumla.

Alisema hivi sasa idadi ya magari na wafanyabiashara katika mji huo inazidi kupungua siku hadi siku na kuhamia sehemu zingine kuwekeza kutokana na vitendo vya vurugu ambazo husababishwa na wanasiasa bila kujali anayeumia ni nani.

“Hivi sasa hakuna mzunguko mzuri wa fedha, wafanyabiashara wakubwa wamekimbioa idadi ya magari yanayovuka katika huu mpaka imepungua kutokana na vurugu zenu vijana ambao mnanyweshwa viloba na kuanza kuandamana mnaharibu mji wenu wenyewe acheni” alisihi Kajuna.

Aliongeza kuwa Mpaka wa Tunduma ni mkubwa kuliko yote nchini na ni kitovu cha uchumi cha Mkoa na Taifa  hivyo kitendo cha kuendekeza vurugu zisizo kuwa na msingi zinasababisha kudorora kwa shughuli za uzalishaji na kupelekea wageni na wawekezaji kukimbia.

Kajuna alienda mbali zaidi na kuwataka Wakazi wa Tunduma kutumia maandamano kuwashinikiza viongozi wa Serikali za Mitaa na Mbunge wao David Silinde kuwasomea mapato na matumizi ya fedha wanazochangishwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo.

Alitoa kauli hiyo kufuatia Mbunge wa jimbo hilo kutuhumiwa kukumbatia fedha za mfuko wa jimbo Milioni 46 bila kuzipeleka katika shughuli za maendeleo ya wananchi na kutatua matatizo yao ikiwemo kero ya maji inayoukabili mji huo kwa muda mrefu.

Alisema Umoja wa Vijana wa CCM unampa siku tatu Mbunge huyo awe amefika Jimboni kwake na kuziwasilisha fedha hizo vinginevyo atachukuliwa hatua za kisheria za kufuja fedha za maendeleo ya wananchi na kuzitumia kwa maslahi binafsi ambapo pia Mbunge huyo inasemekana fedha hizo ametenga ili azitumie kwenye kampeni katika uchaguzi mkuu ujao.

Mbali na tuhuma hizo Mbunge Silinde pia anatuhumiwa kumiliki miradi ya maji ya wananchi na kugeuza kuwa mradi binafsi na kuwatoza fedha pindi wanapotaka kupata huduma ya maji katika visima viwili vilivyochimbwa mjini hapo.

Wakizungumza mbele ya Mwenyekiti huyo, Wakazi wa Mji wa Tunduma walisema kutokana na kero ya maji ambayo inawakabili wakazi hao walikubaliana kuitisha harambee na kuchanga ili kuchimba visima jambo ambalo lilifanikiwa na kupata zaidi ya shilingi Milioni 21 ambazo alikabidhiwa Mbunge Silinde.

Walisema baada ya hapo Visima viwili vilichimbwa lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida visima hivyo vikaandikwa mradi binafsi wa mbunge hivyo kusababisha watu wanaotaka huduma ya maji kuuziwa na fedha kuzichukua yeye kwa shughuli zake binafsi.
 Na Mbeya Yetu

No comments: