Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Sunday, March 8, 2015

WAFANYAKAZI WANAWAKE WA NHIF MKOA WA MBEYA WATEMBELEA HOSPITALI YA WAZAZI META NA KUTOA ZAWADI.

Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiwa wameshika bango lenye ujumbe wa siku ya wanawake duniani kabla ya kutoa msaada katika Hospitali ya Wazazi ya Meta.

Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kutoa msaada.

Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiwa wameshikana mikono kuashiria alama maalum.

Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiwa wamebeba vitu wakipeleka wodini kwa ajili ya msaada kwa wagonjwa.

Muuguzi, Sister Frolence Maisa akiwasaidia Watumishi wanawake wa NHIF kuingiza vitu wodini.

Mtumishi Anotolia Lusasi akizungumza na Muuguzi wa zamu Salome Mpogole walipoenda kutoa msaada katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.


. Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiendelea kukabidhi misaada mbali mbali kwa wagonjwa.



Muuguzi Sister Maisa akisaidia kukatakata sabuni za unga tayari kwa ajili ya kugawa kwa wagonjwa.

Mtumishi akigawa zawadi kwa mgonjwa

Watumishi wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mbeya wakiwa wamemshika mtoto wa Yusta Agustino ambaye ni miongoni mwa watoto sita waliozaliwa usiku wa kuamkia Machi 8, mwaka huu.

Watumishi wakiendelea kutoa msaada.

Sister Maisa akisaidia kugawa vitu kwa wagonjwa.

Mtumishi wa NHIF akiwa amewabeba mapacha waliozaliwa na Happy Michael siku ya Machi 7, mwaka huu walipotembelea wodi namba 2 kwa ajili ya kugawa zawadi katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani.



WATUMISHI wanawake wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) Mkoa wa Mbeya wametembelea Hospitali ya Wazazi Meta na kutoa misaada mbali mbali ikiwa ni kusherekea siku ya wanawake duniani.

Akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo kwa niaba ya Watumishi wenzake, Tuli Mwakyusa, alisema wameguswa na kitendo cha wanawake wenzao kuwa Hospitali na kushindwa kufanya kazi zinazoweza kuwaingizia kipato.

Mwakyusa alisema ili kuadhimisha siku ya Wanawake duniani wameona wakatumia nafasi hiyo kuwafariji wanawake wenzao waliolazwa Hospitalini kutokana na shida mbali mbali sambamba na wengine kujifungua watoto katika siku hiyo.

Mtumishi mwingine wa NHIF, Anatolia Lusasi, alisema si rahisi sana kujua mahitaji ya wanawake waliopo Mahosipatilini pasipo kuwatembelea na kujua shida zao.

“ Tukiwa tunatembea barabarani hatujui wenzetu waliolazwa wanashida gani lakini sisi leo tumekuja tumejionea jinsi hali halisi ilivyo na ndiyo maana tukaona ni vema tukatoa chochote” alisema Lusasi.

Aliongeza kuwa kuna umuhimu mkubwa kwa jamii kujenga utamaduni wa kuwatembelea mara kwa mara wagonjwa walioko Hospitalini kwani ni wengi ambao wanakosa msaada kutokana na kutokuwa na ndugu na jamaa wakuweza kuwapa huduma.

Alisema wakiwa hospitali hapo wamejifunza mambo mbali mbali zikiwemo huduma zitolewazo na Hospitali ya Wazazi Meta hususani kuwahudumia akina mama wanaojifungua pamoja na utunzaji wa watoto wachanga waliozaliwa kabla ya muda kufika.

Aidha aliupongeza uongozi wa Hospitali hiyo kwa jitihada zake za kudumisha usafi wa mazingira pamoja na mawodi ya wagonjwa kuwa masafi na katika mpangilio mzuri jambo alilosema linasaidia mgonjwa kupona haraka kutokana na hali ya usafi.

Alivitaja vitu vilivyopelekwa kuwa ni pamoja na Sabuni za mche  Katoni 5, sabuni za unga boksi 3,Pedi katoni 3 na Nepi dazani 3  vyote vikiwa na thamani ya shilingi Laki moja na nusu.

Alisema mchango huo umetolewa na watumishi wanawake wa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa Mbeya wakiwa sita walioongozana pamoja kuwatembelea wagonjwa hospitalini hapo ambao ni Anatolia Lusasi, Tuli Mwakyusa, Emma Mdoe, Egdia Kyabona, Pendoeva Kapola na Esther Haule.

Akishukuru kwa ajili ya Msaada huo, Muuguzi wa Zamu wa Hospitali ya Wazazi Meta, Salome Mpogole, aliwapongeza watumishi wa NHIF kwa moyo waliounesha kwa kuwatembelea wagonjwa na kutoa msaada huo.

Alisema katika usiku wa kuamkia Machi 8, mwaka huu ambayo ni siku ya Wanawakle duniani katika Hospitali hiyo wamezaliwa watoto sita ambao wote ni wa kike.

Mwisho.
Na Mbeya yetu

No comments: