Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, March 25, 2015

MBEYA YAUNGANA NA DUNIA NZIMA KUADHIMISHA SIKU YA KIFUA KIKUU.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nyerembe Munasa akihutubia wananchi katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.

Mratibu wa Kifua Kikuu Mkoa wa Mbeya akitoa neno la shukrani katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dk. Agnes Buchwa akitoa taarifa ya hali ya maambukizi ya ugonjwa wa Kifua kikuu kwa Mkoa wa Mbeya katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.

Mkuu wa Wilaya pamoja na wageni wengine wakipokea maandamano

Weston Asisya kutoka kituo cha Utafiti Mbeya(MMRP) akitoa burudani kwa kuongoza Brass band ya Kihumbe katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.

Waandamanaji katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.


Kikundi cha Kihumbe kikiongoza Maandamano.

 Waandamanaji wakiwa na mabango katika maandamano ya siku ya Kifua kikuu duniani.

Washiriki katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.


Washiriki katika maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Mtaa wa Kabwe kata ya Iyela Jijini Mbeya.




     

HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya imetajwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Kifua kikuu katika takwimu za Mkoa zilizofanyika Mwaka jana ikilinganishwa na Wilaya zingine.

Aidha katika takwimu hizo zinaonesha jiji la Mbeya kuwa na wagonjwa wengi ambao ni 816 ikifuatiwa na Rungwe yenye wagonjwa 659,Chunya ni ya tatu ikiwa na wagonjwa 571,inafuatia Mbozi yenye wagonjwa 521,Mbarari wagonjwa 516,Kyela 313,Mbeya vijijini 283 na ileje wagonjwa 72.

Hayo yalibainishwa jana na Kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Mbeya Dk.Agnes Buchwa katika maadhimisho ya Kifua kikuu duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika Stendi ya Mabasi Kabwe jijini Mbeya.

Hata hivyo mbali na Jiji la Mbeya kuongoza pia imeonekana ugonjwa huo kukua na kuongezeka kila mwaka ikilinganishwa na hali ilivyokuwa katika miaka ya 2000.

Dk. Buchwa aliongeza kuwa  kwa sasa mkoa wa Mbeya ni moja kati ya mikoa mitano nchini yenye wagonjwa wengi wa kifua kikuu.

Alisema  mkoani hapa wagonjwa wa kifua kikuu waliongezeka kutoka 3,743 mwaka 2000 hadi 3,952 mwaka 2005 lakini baada ya hapo wagonjwa walipungua hadi kufikia 2,949 mwaka 2008.

Alisema baada ya hapo idadi ya wagonjwa imeabza kuongezeka tena ambapo mwaka 2009 wagonjwa walifikia 3,110,mwaka 2010 wakiafikia 3,215 na mwaka 2011 wakafikia 3,418 huku mwaka 2012 wagonjwa wakizidi kuongezeka na kufikia 3,502.

Alisema takwimu za mwaka 2011 zinaoneshya kuwa katika kila watu 100,000 mkoani Mbeya,watu 127 wana kifua kikuu na mwaka 2012 kati ya watu 100,000 watu 129 walipatikana na ugonjwa huo.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Mbeya, Nyirembe Munasa,ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo aliwataka wananchi kujitokeza kupima afya zao na wale wanaobainika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo kuhakikisha wanafika katika vituo vya afya husika kupata tiba kwakuwa huduma hizo hutolewa bure.

Aliongeza kuwa Wananchi wanatakiwa kuhamamishwa na kufundishwa jinsi ya kujikinga na maambukizi mapya ya ugonjwa wa kifua kikuu kwa kuelezwa dalili zake ili kulinda nguvu kazi ya taifa.

Katika maadhimisho hayo Baadhi ya waathirika wa ugonjwa wa kifua kikuu waliotibiwa na wanaoendelea kutibiwa walishauri wagonjwa wa ugonjwa huo kuzingatia masharti ya tiba ili kuepukana na usugu wa ugonjwa unaoweza kuhatarisha zaidi maisha yao.

Mwisho.
Na Mbeya yetu

No comments: