Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, November 24, 2014

KAMPUNI YA MABATI YA ALAF YATOA MSAADA WA MABATI KWA AJILI YA UJENZI WA MAABARA ZA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA MBEYA.

 Meneja wa Kampuni ya ALAF Tawi la Mbeya, Greyson Mwakasege akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya kabla ya kumkabidhi msaada wa mabati 384 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa maabara.
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigallah King, akitoa shukrani kwa kampuni ya ALAF  kwa kujitolea mabati kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa maabara kwa shule za sekondari za Wilaya ya Mbeya.
  Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigallah King na Meneja wa ALAF tawi la Mbeya, Greyson Mwakasege wakikabidhiana mabati 284 kwa ajili ya ujenzi wa maabara katika shule za sekondari za Kata.
 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigallah King akiwaonesha waandishi wa habari(hawapo pichani) msaada wa mabati aliyokabidhiwa na Kampuni ya ALAF .
 Meneja wa ALAF tawi la Mbeya, Greyson Mwakasege akimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Mbeya bidhaa zingine zinazozalishwa katika kiwanda cha Mbeya.

 Fundi umeme na mtaalamu wa Mashine wa Kiwanda cha kuzalisha mabati, Himid Mwenzegule akiendelea kuendesha mitambo ya mashine ya kuzalisha mabati kiwandani hapo.
 Mashine ya kuzalisha mabati ya migongo ya kawaida aina ya Corrugator ikiendelea na kazi.
 Mashine ya kuzalisha mabati ya migongo mikubwa aina ya IT.
 Mashine ya kuzalisha vigae aina ya Versa Tile
 Mabati aina ya Simba Dumu yaliyozalishwa kiwandani hapo.
 Baadhi ya mabati yaliyozalishwa kiwandani hapo yakiingizwa kwenye Roli tayari kuelekea sokoni kwa wateja.


KAMPUNI ya mabati ya ALAF imetoa  msaada wa mabati 384 kwa ajili ya ujenzi wa maabara za shule za Sekondari za Wilaya ya Mbeya zenye thamani ya shilingi Milioni 7.
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigallah King,Meneja wa Tawi la Mbeya Greyson Mwakasege, alisema walipokea maombi kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbeya kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa maabara katika Shule za Kata.
Alisema walikubaliana na ombi hilo na kuona ni vema kusaidia Bandle 32 sawa na mabati 384 yenye thamani ya Shilingi Milioni 7 baada ya mabati hayo kuanza kuzalishwa katika Kiwanda cha Mbeya ambacho pia kinahudumia Mikoa ya Ruvuma, Katavi, Rukwa,Njombe, Iringa na Mbeya.
Alisema ni matarajio yao ya kuendelea kusaidia maeneo mengine kama mchango wa Kampuni kwa jamii inayowazunguka pamoja na kuthamini wateja wake ambao hupata huduma kutoka katika kiwanda cha Mbeya.
Mwakasege aliongeza kuwa katika Kiwanda cha Mbeya kina mashine tatu ambazo ni Mashine aina ya IT inayotengeneza mabati ya migongo mikubwa, Mashine aina ya Corrugator inayozalisha mabati yenye migongo ya kawaida midogo pamoja na mashine aina ya Versa Tile inayozalisha vigae aina ya Versa.
Alizitaja bidhaa zingine zinazopatikana kuwa ni pamoja na Bati za Afrika kusini na vigae vyenye rangi za Bluu, Kijani na Nyekundu,Nondo kutoka Uturuki, Black Pipe, Z parlin na Hollow section.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Dk. Norman Sigallah King, mbali na kutoa shukrani kwa Kampuni ya ALAF  kwa msaada wa mabati pia alitoa wito kwa wafanyabiashara wa Wilaya ya Mbeya kujenga utamaduni wa kuchangia shughuli za maendeleo ya Wilaya.
Alisema mabati hayo yatasaidia katika ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Galijembe ambayo imeteuliwa na Wilaya kuwa Shule ya Bweni ya wasichana kutokana na ujenzi wa maabara kukamilika kwa asilimia kubwa.
Alisema lengo la kuiteua shule ya Galijembe kuwa shule ya Wasichana ya bweni ya Wilaya ni kuwaondolea adha watoto wa kike ambao asilimia kubwa wanaumri mdogo kwenda uaraiani kupanga vyumba baada ya kufaulu kujiunga na sekondari.
Alisema wasichana wanapata madhara makubwa wakiwa wamepanga kwenye nyumba uaraiani yakiwemo Mimba za utotoni na magonjwa ikiwa ni pamoja na kupunguza hali ya ufaulu darasani kutokana na mazingira hivyo Wilaya ya Mbeya imejipanga kuhakikisha hilo linaondoka.


No comments: