Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, August 27, 2014

KERO KATIKATI YA JIJI LA MBEYA: MACHINGA WAJIACHIA WAPANGA BIDHAA MPAKA BARABARANI , WAHUSIKA WAMEUCHUNA, JE MAPATO HAYA YANAENDA WAPI? NA NI SAHIHI HAWA WATU KUWA HAPA?

Imekuwa ni moja ya kero kubwa na uchafuzi wa jiji katika Lango la Jiji eneo ambalo wageni , Viongozi wakubwa na watu mbalimbali wanapita.
Kero hii ambayo wahusika mnaliona hili na mnalikalia kimya linawapa watu maswali mengi sana na mpaka kudhania labda ni kamradi kamtu na ambako hakaeleweki eleweki kuwa pato lake linaenda wapi
Sio pengine ni kakipande tuu kutoka Eneo la Benki ya CRDB hadi Eneo la BP kona ya kuelekea Posta. Inafahamika kuwa eneo hili lilikatazwa kufanyika biashara lakini sasa imekuwa ndio eneo la watu kuweka Bidhaa zao na kila siku watu hawa wanazidi
Je Wahusika mpo na mnalizungumziaje?
 Hapa kila mtu anaweka Bidhaa zake wenye Nguo , Viatu na vitu mbalimbali wote wapo hapa
 Kila mmoja yupo Huru tuu
 Hapa ni nje ya wakusanya mapato(TRA) wanakazana kufukuza watu wengine maeneo mengine je hawa hawawaoni? 
 Pamegeuka Duka
 Kila kitu kinapatikana eneo hili
 Hii njia ya kuelekea Posta unakaribishwa na Viatu 
 Wengine ndio kwanza wanaanza weka mzigo
 Kila mmoja anawahi kuanza biashara
 Wale Mgambo wa Jiji ina maana hapa hawakupangiwa kupita?
 Wadau hili si ni Duka kabisa!
 Je sasa hapa hawa ni Machinga ama wafanya biashara?
Hata bei zao ukigusa hapa sio za Machinga....

Ndugu Mdau na Msomaji wa Mbeya yetu... Toa maoni yako Juu ya Hili...

Picha na Mbeya yetu

2 comments:

Anonymous said...

I think lack of awareness on part of the society. leaders mayor,devl. director AND TRA share big chunk of blems.plse enforce the laws!!!I think lack of awareness on part of the society. leaders mayor,devl. director AND TRA share big chunk of blems.plse enforce the laws!!!Washington DC USA

Anonymous said...

that is Tanzania
corrupted country..