Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Sunday, July 13, 2014

RAIS KIKWETE MGENI RASMI KATIKA SHEREHE ZA MIAKA 75 YA KANISA LA TAG JIJINI MBEYA.

Kutoka kushoto ni Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali katikati ni Rais Dkt Jakaya Kikwete na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abbas Kandoro , wakiwa wanaimba wimbo wa Taifa kabla ya Sherehe kuanza Rasmi.
 Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali  akitoa salam za Shukurani kwa Mgeni Rasmi Dkt Jakaya Mrisho Kikwete pia kutoa Historia ya kanisa la TAG toka lilipoanza mpaka sasa linatimiza Miaka 75.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia maelfu ya wananchi kwenye kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa la Tanzania Assemblies of God katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya  Julai 13, 2014
 Baadhi ya Viongozi wa Chama na Serikali wakiwa katika maadhimisho hayo 
 Charles Mwakipesile akiwatunza watoto baada ya kusoma Bibilia kwa umakini kutoka kichwani
 Sherehe zimepamba moto
 Baadhi ya Wageni waalikwa kutoka Nje ya nchi waliokuja kuhudhuria Miaka 75 ya TAG
 Ankali Issa Michuzi katika Sherehe hizo za Miaka 75 ya TAG
 Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali katikati akiwa anazungumza jambo wakati walipokuwa wakijiandaa kutoa zawadi mbalimbali.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizindua kitabu cha Tanzania Assemblies of God (TAG) akiwa na Askofu Mkuu wa TAG Dkt Barnabas Weston Mtokambali wakati wa kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa hilo katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya  Julai 13, 2014
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikabidhiwa tuzo na Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God (TAG) Dkt Barnabas Weston Mtokambali wakati wa kilele cha Sherehe za Miaka 78 ya kanisa hilo katika uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya leo Julai 13, 2014

 Baadhi ya wadau
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Baadhi ya Viongozi wa Kanisa la TAG kutoka Marekani 
 Watoto wakitoa Burudani 


Picha ya Pamoja baada ya Sherehe kumalizika
Picha zote na Mbeya yetu.

No comments: