Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, April 4, 2014

BAADHI ya wananchi wanaouguza ndugu zao katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya wamelalakia kitendo cha uongozi wa Hospitali hiyo kuwafukuza mawodini


Hospitali ya Rufaa ya Mbeya 
Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Aisha Mtanda, alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kuongeza kuwa tatizo hilo ni la muda muda mrefu lakini changamoto ni upungufu wa fedha wa kuweza kutenga eneo la kupumzikia wanaouguza wagonjwa wao.


Baadhi ya Ndugu ya za wagonjwa wakiwa wamelala nje kusubiri muda wa kuwaona ndugu zao waliolazwa hospitalini hapo


Hii ndiyo hali halisi nje ya hospitali hiyo miti yageuzwa kamba ya kuanikia nguo


Baadhi ya ndugu na jamaa wakisubiri muda wakuingia kuwaona ndugu zao


BAADHI ya wananchi wanaouguza ndugu zao katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya wamelalakia kitendo cha uongozi wa Hospitali hiyo kuwafukuza mawodini bila kuwa na utaratibu wala mahali pa kusubiri na kuishi wakati ndugu zao wakitibiwa.

Wananchi hao wanaotoka maeneo tofauti nje na ndani ya Mkoa wa Mbeya wamekuwa wakilala nje ya Hospitali hiyo kutokana na wengi wao kukosa mahala pa kuishi hali inayowapelekea kuhatarisha maisha yao kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha mkoani hapa.

Wakizungumza na Mbeya yetu  baadhi ya wananchi waliokutwa wamelala kando kando ya Hospitali hiyo walisema wanapata usumbufu mkubwa na wanalazimika kulala nje kwa sababu wanafukuzwa wodini ili hali wanajua ni wageni na wagonjwa wao wanatakiwa kupewa huduma za chakula na usafi nje ya Hospitali.

Mmoja wa wananchi hao, Justina Aswile mkazi wa Kapugi Wilaya ya Rungwe, ambaye anamuuguza ndugu yake alisema tangu apewe rufani katika Hospitali ya Wilaya ya Rungwe Makandana hana hata ndugu wa kukaa kwake bali analazimika kukesha nje kusubiria muda wa kuona wagonjwa ndipo aingie Wodini.

Alisema ni bora serikali ama hospitali hiyo ikajenga eneo la kupumzikia wanaouguza ndugu zao ili wapate sehemu ya kupikia baadhi ya vyakula ili kuondoa usumbufu na gharama kubwa zinazowakabili ikiwemo kulazimika kununua chakula wakati wanauwezo wa kupika.

Mwananchi mwingine Kufimba Kalinga alisema anamuuguza baba yake mzazi tangu Februari 19, mwaka huu na tangu hapo amekuwa akilazimika kulala kwa kuomba omba kwa watu mbali mbali jambo ambalo linamletea usumbufu kutokana na kukosa uhuru wa kumuandalia chakula mgonjwa wake.

Walisema wanaiomba serikali kuwajengea sehemu ya kupumzikia na kulala kama zilivyo Hospitali zingine zilizotenga majengo maalumu yanayowasaidia kulala na kuandaa chakula kwa ajili ya wagonjwa wao.

Kwa upande wake Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Aisha Mtanda, alikiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kuongeza kuwa tatizo hilo ni la muda muda mrefu lakini changamoto ni upungufu wa fedha wa kuweza kutenga eneo la kupumzikia wanaouguza wagonjwa wao.

Mtanda alisema hivi sasa uongozi wa Hospitali una mpango wa kuboresha moja wapo ya majengo yaliyopo ndani ya hospitali ili yasaidie kupumzikia kutokana na mazingira wanaishi wananchi hao kuwa magunjwa na hatarishi kwa magonjwa mbali mbali ikiwemo kupata madhara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Aliongeza kuwa wanatarajia kuomba msaada kwa wadau mbali mbali ili waweze kujenga eneo la kupumzikia watu hao ikiwemo Halmashauri ya Jiji la Mbeya  kuwapatia eneo la nje ya Hospitali litakalowasaidia kuandaa vyakula na shughuli zenye msaada kwa wagonjwa wao.

Mwisho.  

Na Mbeya yetu

No comments: