Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, March 7, 2014

Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania (UWAMATA) kanda ya Mbeya wamelalamikia Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani na Mamlaka ya udhibiti wa nchi kavu na Majini(SUMATRA) Mkoa wa Mbeya kwa kuwanyanyasa wawapo kazini.

Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya, Robert Mayala, alisema amepokea malalamiko yao na kwamba Jeshi la Polisi litakutana na Askari wanaolalamikiwa hasa wa Wilaya ya Rungwe na amemwagiza Mkuu wa usalama Barabarani kurekebisha kasoro zote ili kila upande ufanye kazi kwa amani.

Mkuu wa Usalama Barabarani, Butusyo Mwambelo, alikanusha kuwafukuza madereva ofisini kwake bali alidai kuwa viongozi wanatetea wahalifu hali hiyo isipodhibitiwa itasababisha ajali ambazo zinaweza kuepukika.

Ofisa Mfawidhi wa SUMATARA kanda, Amani Shamaje


Mwenyekiti wa Madereva kanda ya Mbeya, Damas Mwandumbya, katika mkutano baina yao na viongozi  uliofanyika katika ukumbi wa Miami uliopo  Ilomba Jijini Mbeya

Mwandumbya akisoma risala yao kwa mgeni rasmi




Baadhi ya viongozi wa madereva toka wilaya zote za mkoa wa Mbeya walihudhuria kikao hicho


Umoja wa Madereva wa Mabasi Tanzania (UWAMATA) kanda ya Mbeya wamelalamikia Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani na Mamlaka ya udhibiti wa nchi kavu na Majini(SUMATRA) Mkoa wa Mbeya kwa kuwanyanyasa wawapo kazini.

Malalamiko yao yalitolewa jana na Mwenyekiti wa Madereva kanda ya Mbeya, Damas Mwandumbya, katika mkutano baina yao na viongozi  uliofanyika katika ukumbi wa Miami uliopo  Ilomba Jijini Mbeya mbele ya Mgeni rasmi Kaimu Kamanda wa  Polisi Mkoa Robert Mayala ambaye piani  Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya.


Mwandumbya akisoma risala yao kwa mgeni rasmi alisema wanaotuhumiwa kula rushwa ni pamoja na Askari Polisi wa kikosi cha Usalama Barabarani wa Wilaya za Rungwe na Mbeya ambao waliwataja kuwa ni   Jane,Vaileth, Shabani, Denis, Hezron na Azimio pamoja na Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa wa Mbeya, Butusyo Mwambelo, ambaye imedaiwa kuwapa malengo Askari wake ili mgao afikishiwe Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya.


Aliongeza kuwa Mgao mwingine wa pesa hizo umetajwa kwenda kwa Mkuu wa Usalama Barabarani nchini na kila Dereva anapokamatwa au kusimamishwa hulazimika kutoa shilingi elfu tano katika kila kituo anachosimamishwa ndipo gari huendelea na safari.


Alisema hali hiyo husababisha Madereva kujaza abiria kupita kiasi  ili kukidhi malengo ya waajiri na kumudu kulipa Askari wa Usalama Barabarani na kama wasipotoa hukamatwa na kutozwa faini au kupelekwa mahabusu hali inayowafanya kufanya kazi katika mazingira magumu.


Aidha Madereva hao walimtuhumu Mkuu wa Usalama Barabarani Mkoa Mbeya kwa kuwafukuza ofisini kwake na kuwa na lugha chafu inayowadhalilisha madereva hali inayopelekea kugoma au kutishia kugoma kutokana na kauli za kiongozi huyo kwa lengo la kushinikiza kuondolewa Mkoani Mbeya.


Mbali ya shutuma hizo kwa Jeshi la Polisi pia Madereva hao walitupia lawama SUMATRA  kwa kuruhusu magari ya aina ya Noah ambayo yameanza kusafirisha abiria bila kukidhi vigezo hali inayosababisha baadhi ya magari ya abiria aina ya Hiace kushindwa kufanya kazi kutokana na magari hayo kufanya kazi kiholela huku Jeshi la Polisi na SUMATRA wakifumbia macho.


Akijibu risala yao ambayo ilijaa tuhuma, Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Mbeya Robert Mayala aliwapa fursa wanaotuhumiwa kujieleza mbele ya mkutano huo uliojumuisha madereva ili kujiridhisha na majibu.


Mkuu wa Usalama Barabarani, Butusyo Mwambelo, alikanusha kuwafukuza madereva ofisini kwake bali alidai kuwa viongozi wanatetea wahalifu hali hiyo isipodhibitiwa itasababisha ajali ambazo zinaweza kuepukika.

Aidha alikiri kupokea changamoto na mapungufu aliyoelezwa na madereva hayo kwa madai kuwa atayafanyia kazi na yeye mwenyewe atajirekebisha ili kuendelea kudumisha hali ya usalama barabarani pamoja na abiria.


Kwa upande wake Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya, Robert Mayala, alisema amepokea malalamiko yao na kwamba Jeshi la Polisi litakutana na Askari wanaolalamikiwa hasa wa Wilaya ya Rungwe na amemwagiza Mkuu wa usalama Barabarani kurekebisha kasoro zote ili kila upande ufanye kazi kwa amani.


Alihitimisha kwa kuwataka Madereva kutii sheria bila shuruti ili kuepusha ajali na kuwataka madereva wakatae kutoa rushwa na Askari atakaye walazimisha watoe taarifa kwake kwa hatua zaidi.

Na Mbeya yetu


No comments: