Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, January 31, 2014

SHAHIDI wa tatu katika Kesi inayowakabili Maaskari wawili na Raia watatu ya unyang’anyi wa kutumia Siraha, Pasupuret Sreedhar ambaye ni raia wa India na Mhanga wa tukio hilo ameiambia Mhakama jinsi washtakiwa walivyofanikiwa kuwateka na kuwapora mali zao.




SHAHIDI wa tatu katika Kesi inayowakabili Maaskari wawili na Raia watatu ya unyang’anyi wa kutumia Siraha, Pasupuret Sreedhar ambaye ni raia wa India na Mhanga wa tukio hilo ameiambia Mhakama jinsi washtakiwa walivyofanikiwa kuwateka na kuwapora mali zao.

Akizungumza katika kesi hiyo huku akiongozwa na Wakili wa upande wa Jamhuri, Basilius Namkambe mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mbeya, Michael Mteite, Shahidi huyo ambaye hakuweza kuzungumza Kiswahili kabisa hali iliyopelekea Mahakama kumtafuta Wakili maarufu Mkoani Mbeya, Sambwee Shitambala kuwa Mkalimani wake aliweza kuwatambua Watuhumiwa wote watano.

Shahidi huyo aliiambia Mahakama hiyo kuwa Mnamo Januari Mosi Mwaka huu aliwasili Jijini Dar Es Salaam akitokea kwao Nchini India akitumia usafiri wa ndege wa Shirika la Oman akiwa na lengo la kufuatilia mradi wa Uchimbaji dhahabu katika Migodi ya Chunya Mkoani Mbeya inayoendeshwa na kampuni yao ya Otro Mining.

Alisema Januari 3,Mwaka huu alisafiri kutoka Dar Es Salaam kuja Mbeya akitumia Shirika la Ndege la Precision ambapo aliwasili majira ya Saa Saba na Nusu Mchana na kupokelewa na rafiki yake Isaya Mkindi ambaye walielekea naye moja kwa moja hadi Mbeya Hotel alikopata chakula cha Mchana.

Alisema baada ya hapo alipewa Dereva aliyemtaja kwa jina la Ezekia ambaye alimpeleka Mwanjelwa kununua Mablanketi mawili kisha kurudi katika Ofisi ya Rafiki yake huyo ambapo ilipofika majira ya Saa 10:45 jioni walianza safari ya kuelekea Chunya akiwa na rafiki yake pamoja na dereva Ezekia.

Alisema wakiwa njiani walipofika katika Milima ya Kawetere kilomita 20 kutoka Mbeya Mjini walikuta magari mawili yakiwa yameachana kwa mita 200 ambapo walilipita gari moja na ndipo walipokaribia gari lingine wakakutana na vijana Wanne ambao mmojawapo aliwasimamisha na kuomba msaada wa Spana ya kufungulia tairi ya gari yao wakidai kuwa inapancha.

Baada ya kueleza hivyo Wakili wa Serikali aliiomba Mahakama imruhusu Shahidi huyo kama anaweza kuwatambua Watuhumiwa jambo ambalo alitekeleza kwa kuwagusa Mshtakiwa namba moja, Tatu, Nne na Tano kisha kuendelea na kutoa maelezo kuhusu kilichoendelea baada ya kuombwa spana.

Shahidi huyo aliendelea kusema kuwa baada ya Dereva wake kuwajibu kuwa hawana spana ndipo Mtuhumiwa namba tatu ambaye ni Askari Magereza alipotoka na kurudi akiwa na pingu mkononi na kumfunga Dereva kisha kumshusha kwenye gari na kuelekea naye kwenye gari yao ndogo.

Aliongeza kuwa baada ya kufanya hivyo walimshika yeye huku wakimuoneshea panga na kumwamuru asiongee neno lolote kisha kuhamisha mizigo kwenye gari na kupeleka kwenye gari yao ambayo li Kompyuta za Mkononi mbili, begi, mablanketi na Simu za Mkononi ambazo kabla hawajachukua alikuwa ameshawasiliana na Mwenzie aliyoko Chunya aliyemtaja kwa jina la Jamir Amar.

Alisema akiwa ameshikwa na kuongeleshwa na watu hao simu yake ilikuwa ikisikika na wenzie ambao waliweza kutoa taarifa katika Jeshi la Polisi ambalo lilifanikiwa kuwakamata muda mfupi baada ya watu hao kutokomea na vitu vyao na baada ya wao kuachwa akiwemo Dereva aliyekuwa amefungwa pingu kuachiwa.

Hata hivyo Wakili wa utetezi katika kesi hiyo Ladislaus Lwekaza alimuuliza Shahidi huyo kama kweli aliwaona watuhumiwa wakiwa eneo la tukio na siyo kalishwa maneno alijibu anawafahamu kwa sababu aliwaona wakifanya tukio kwa sababu ilikuwa jioni kabla jua halijazima.

Wakili Lwekaza aliongeza kuwa akiruhusiwa kuwabadilisha watuhumiwa mkao wao anaweza kuwatambua Shahidi huyo alijibu anaweza hivyo akatakiwa kutoka nje ili waweze kuwachanganya ndipo awatambue jambo ambalo lilipingwa na Wakili wa Serikali kuwa haijawahi kutokea utambuzi ukafanywa wakati kesi inaendelea kusikilizwa na kuongeza kuwa jambo hilo hufanyika kipindi cha upelelezi.

Kutokana na hoja hizo Hakimu Mteite alikubaliana na hoja ya upande wa Mashtaka hivyo kutupilia mbali maombi ya upande wa mashtaka ya kumtaka Shahidi atoke nje ili wamchanganyie watuhumiwa kwa ajili ya kuwatambua  na kuamuru kuendelea na maswali mengine.

Watuhumiwa hao ni pamoja na Mshitakiwa namba moja ambaye ni Askari Polisi PC James mwenye namba F8302 wa Wilaya ya Mbeya ambaye kabla ya kufikishwa mahakamani alivuliwa Uaskari baada ya kuhukumiwa kijeshi.

Wengine kuwa ni mshtakiwa namba mbili kuwa ni Elinanzi Mshana(22)Mkazi wa Iyela Jijini Mbeya, Askari Magereza mwenye namba B 500 Sajenti Juma Mussa(37) wa Gereza la Ruanda Mbeya,Mbaruku Hamis(29) Mkazi wa Iyela na Amri Kihenya(38) Mkazi wa Iyela.

Akisoma mashtaka yao Mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite, Basilius Namkambe alisema watuhumiwa hao walitenda kosa hilo Januari 3, Mwaka huu majira ya saa 11 jioni katika eneo la Mlima Kawetere barabara ya Mbeya Chunya.

Alisema watuhumiwa hao kwa pamoja walitenda kosa hilo kwa kulizuia gari aina ya Pick Up lililokuwa likiendeshwa na Ezekia Matatira (34) Mkazi wa Iyunga Jijini Mbeya ambaye alikuwa na mtu aliyekuwa akifahamika kwa jina la Sreedhar Pasupelet(38) mwenye asili ya Kiasia wakitumia magari madogo mawili ambayo ni GX 100 Toyota Cresta T 782 BEU na Gari linguine ambalo lilikuwa na namba za Chesesi GX 6011832 aina ya Grand Mark II.

Hata hivyo Kesi hiyo iliahirishwa hadi Februari 13, Mwaka huu itakapoendelea tena kwa upande wa mashtaka kuwaleta mashahidi wake.

Na Mbeya yetu

No comments: