Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, January 24, 2014

ASHINDWA KUENDELEA NA MASOMO AKIHOFIA KUZOMEWA BAADA YA KUDAIWA KULAWITIWA NA MWALIMU MKUU.


Huyu ndiye mwanafunzi aliyekuwa anatendewa ukatili huo

Hii ndiyo ofisi ya mwalimu mkuu huyo ambayo ilikuwa inatumika kwa matendo machafu ya mwalimu huyo


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema atalifanyia kazi kutokana na kutokuwa Ofisini kwa wakati huo na kulitolea ufafanuzi unaotakiwa.

Ofisini kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya Mbeya

 Afisa Elimu Msingi wa Wilaya ya Mbeya, Dionice Boay alipoulizwa kuhusiana na tuhuma za Mwalimu wake alikiri kuzipata na kuongeza kuwa kutokana na Mwalimu huyo kufikishwa katika vyombo vya Sheria wao kama Ofisi hawana cha kufanya zaidi ya kusubiri Ripoti ya Polisi ambapo Mwalimu atachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma.
                                                                           

MWANAFUNZI mmoja (Jina limehifadhiwa umri wake ni 16) wa Darasa la Saba katika  Shule ya Msingi Mkombozi iliyopo katika mji mdogo Mbalizi Wilaya ya Mbeya Mkoani hapa ameshindwa kuendelea na masomo tangu shule zifunguliwe akiogopa kuzomewa na wenzie baada ya kuhisiwa kulawitiwa na Mwalimu Mkuu wake.

Hatua ya mwanafunzi huyo kushindwa kufika shuleni kuungana na wenzie kumetokana na madai ya kuzagaa kwa tuhuma za Mkuu wake wa shule kumwingilia kimwili mwanafunzi huyo mwenye jinsia ya kiume wakati wa masomo ya jioni(Twisheni).

Akizungumza na waandishi wa habari Mwanafunzi huyo alisema Mwalimu wake huyo ambaye alimtaja kwa jina  la Lusekelo Thom, kuwa anatabia ya kumbakiza yeye peke yake baada ya muda wa masomo ya jioni kuisha na ndipo huenda naye ofisini na kuanza kumvua nguo.

Alisema tatizo hilo limedumu kwa kipindi kirefu tangu Aprili Mwaka jana hadi Disemba 27, mwaka jana baada ya bibi anayemlea kugundua (jina limehifadhiwa kwa ajili ya upelelezi) katika mahojiano kutokana na mwanafunzi huyo kuchelewa kurudi nyumbani kila siku tofauti na wengine.

Kwa mujibu wa majirani wa Mwanafunzi huyo walisema kugundulika kwa maovu anayofanyiwa na mwalimu wake kulitokana na upotevu wa fedha shilingi 20,000 na ndipo bibi huyo alipomuona mjukuu wake akiwa na mkebe mpya na ndipo alipomuuliza kuhusu fedha zake ambapo Mwanafunzi huyo alikataa kabisa.

Walisema baada ya kubanwa zaidi alidai fedha za kununulia mkebe alipewa na Mwalimu wake na amekuwa na kawaida ya kumpa fedha mwanafunzi huyo kila siku ikiwa ni pamoja na kumwambia asilipe ada ya masomo ya jioni kwa madai kuwa atakuwa anamlipia.

Alipobanwa zaidi mwanafunzi huyo alidai kuwa baada ya kupewa fedha na mwalimu huyo huenda naye ofisini na kufunga mlango kisha huvua nguo zake na kumwamuru naye avue na kumlazimisha ashike nyeti za mwalimu wake huku mwalimu naye akimshika shika na huo mchezo ulikuwa ukifanyika kila siku na baada ya hapo mwalimu alikuwa akimrudisha mwanafunzi kwa bibi yake majira ya saa mbili usiku.

Mashuhuda wa tukio hilo na baadhi ya walinzi wa shule hiyo walikiri kuwepo kwa tuhuma za udharirishaji wa Mwalimu huyo kwa Mwanafunzi kwa madai kuwa kila siku Mwalimu huyo kujifungia ofisini na mwanafunzi ikiwa ni pamoja na kuongozana naye kila mara.

Aidha baadhi ya ndugu walisema baada ya kubaini hali hiyo walienda kutoa taarifa katika kituo kidogo cha Polisi cha Mbalizi ambapo Jeshi la Polisi lilimkamata Mwalimu huyo Januari 4, Mwaka huu na kufanya naye mahojiano kisha kumpeleka mwanafunzi huyo Hospitalini kwa ajili ya vipimo.

Hata hivyo Mwalimu huyo alipohojiwa kuhusiana na tukio hilo alikataa kuhusika huku majibu ya vipimo vya Hospitali vikionesha kutokuingiliwa kimwili kwa mwanafunzi ingawa Maelezo ya mtoto alidai kuchezewa nyeti zake kila siku na kwamba suala la kuingiliwa kimwili alikuwa akilazimishwa lakini hakuweza kufanikiwa.

Mwalimu huyo aliachiwa na jeshi la Polisi katika kituo kidogo cha Mbalizi alipokuwa ameshikiliwa kwa ajili ya mahojiano baada ya kuwekewa dhamana na Mratibu wa Elimu kata ya Utengule Usongwe, Fredrick Silumbwe, na kwamba upelelezi bado unaendelea ili kubaini kama kweli mwalimu huyo anafanya vitendo hivyo huku kukiwa na taarifa kuwa Mwalimu huyo baada ya tukio hilo alisafiri na kuelekea Kibaha Mkoani Pwani ambako yuko hadi sasa.

Kwa upande wake Mratibu Elimu kata alipoulizwa kuhusiana na tuhuma dhidi ya mwalimu wake alisema hata yeye amekuwa anazisikia mitaani na kuhusu kuweka dhamana alikiri kwa madai kuwa alipigiwa na baadhi ya walimu na ndipo alipofanya hivyo kutokana na dhamana ni haki ya kila mtu.

Naye Afisa Elimu Msingi wa Wilaya ya Mbeya, Dionice Boay alipoulizwa kuhusiana na tuhuma za Mwalimu wake alikiri kuzipata na kuongeza kuwa kutokana na Mwalimu huyo kufikishwa katika vyombo vya Sheria wao kama Ofisi hawana cha kufanya zaidi ya kusubiri Ripoti ya Polisi ambapo Mwalimu atachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za utumishi wa umma.

Alisema kama ofisi hatua ya kwanza ni kumsimamisha kazi na kuteua Mwalimu mwingine kukaimu Ukuu wa Shule ya Msingi Mkombozi wakati ofisi ikisubiri taratibu za Kimahakama kutokana na tatizo hilo kuegemea kwenye makosa ya jinai.

Aliongeza kuwa Ofisi pia inatarajia kufanya ukaguzi katika shule hiyo ili kubaini kama Mwalimu alikuwa na makosa mengine na kujua sababu ya Mwanafunzi kutoenda shule hadi sasa licha ya wenzie kuendelea na masomo.

Hata hivyo Kituo cha Haki za Binadamu kilionesha mshangao kutokana na mtuhumiwa wa tukio hilo kuachiwa kwa dhamana ili hali upelelezi haujakamilika na hakuna hatua zozote ambazo Jeshi la Polisi linaonesha kulifanyia kazi ambapo mtuhumiwa alifikishwa Polisi Januari 4, Mwaka huu.

Mwenyekiti wa Kituo cha Haki za Binadamu Mkoa wa Mbeya, Said Madudu alisema Jeshi la Polisi limechukulia suala hili kama ni siasa kwa kuchelewa kuchukua hatua kwa wakati huku mtoto akiendelea kukosa haki yake ya msingi ya masomo.

Aidha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema atalifanyia kazi kutokana na kutokuwa Ofisini kwa wakati huo na kulitolea ufafanuzi unaotakiwa.

Hata hivyo uchunguzi uliofanywa umebaini kuwepo kwa rushwa zinazopelekea upelelezi wa kesi hiyo kuchelewa kutokana na kuwepo kwa taarifa za Mtuhumiwa kutoa fedha shilingi Milioni Tatu ambazo bado haijulikani mgao wake uliwagusa akina nani.



Na Mbeya yetu

No comments: