Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, November 25, 2013

MZEE ALIYEPONA KUZIKWA HAI AELEZEA KISA KIZIMA

Mzee huyo Pascal Mwanjelanje(75) alinusurika kuzikwa akiwa hai akituhumiwa kumuua mke wa mtoto wake aliyejulikana kwa jina la Salome Amosi (20).
Kaburi ambalo angezikwa huyo mzee
Mume wa Marehemu, Moses Pascal (27) mkazi wa Uyole Jijini Mbeya alisema mkewe alifikwa na umauti walipokuwa wameenda kijijini kwao Shilanga kwa ajili ya kilimo lakini kabla ya kifo cha Mkewe walikuwa wametoka Hospitali kumtibu mtoto wao majira ya saa Tisa alasiri.
Mwenyekiti wa kijiji cha Shilanga, Romani Tubuke, alisema lilitokea hivi karibuni majira ya saa 9 alasiri wakati marehemu Salome Amosi (20) kupoteza maisha akiwa anafua nguo katika mto uliojirani na kijiji hicho.



Mzee mmoja mkazi wa kijiji cha Shilanga Wilaya ya Mbeya Mkoani hapa amenusurika kuzikwa akiwa hai akituhumiwa kumuua mkwewe kwa ushirikina.

Tukio lilitokea hivi karibuni majira ya saa tisa alasiri ambapo Mzee huyo Pascal Mwanjelanje(75) alinusurika kuzikwa akiwa hai akituhumiwa kumuua mke wa mtoto wake aliyejulikana kwa jina la Salome Amosi (20).

kupona kwa mzee huyo kumetokana na kugoma kwenda sehemu lilipochimbwa kaburi kwa ajili ya mazishi ya marehemu baada ya kushtukia mchezo mchafu wa vijana waliokuwa wakichimba kaburi.

mzee huyo alishtukia kufuatia tukio la awali lililotokea Novemba 6, Mwaka huu katika kijiji cha Mshewe Wilayani hapa ambapo watu Sita akiwemo Mwenyekiti wa kijiji walipandishwa mahakamani wakituhumiwa kumzika mtu akiwa hai wakimtuhumu kumuua mwanaye kwa ushirikina.


Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa kijiji cha Shilanga, Romani Tubuke, alisema lilitokea hivi karibuni majira ya saa 9 alasiri wakati marehemu Salome Amosi (20) kupoteza maisha akiwa anafua nguo katika mto uliojirani na kijiji hicho.

Alisema baada ya kupata kwa taarifa za msiba huo familia iliandaa matanga kama kawaida ambapo siku iliyofuata vijana wa kuchimba kaburi walianza kuchimba majira ya saa sita mchana ambapo kabla ya kukamilisha walisitisha zoezi hilo na kisha kuandamana hadi walipowaombolezaji na kuwasihi wanyamaze.

Alisema baada ya watu wote kukaa kimya ndipo vijana hao walipohoji sababu ya kifo cha marehemu na kutaka majibu ya kuridhisha ili wakaendelee na shughuli za machimbo ambapo walianza kumuuliza bibi aliyemlea marehemu ambaye aliulizwa kama mjukuu wake amewahi kuwa na tatizo lolote lakini alijibu kuwa mjukuu wake hakuwahi kusumbuliwa na ugonjwa wowote.

Alisema kutokana na majibu ya bibi huyo vijana hao walimsimamisha pia Mume wa Marehemu Moses Pascal(27) ambaye alisema yeye binafsi hajui ugonjwa uliomuua mkewe zaidi ya kuletewa taarifa kuwa amekufa mtoni akiwa anafua baada ya yeye kuachiwa mtoto nyumbani.

Hata hivyo vijana hao hawakuridhika na majibu hayo na kuamua kumwita mzee Pascal Mwanjilanji wakitaka aeleze sababu za kifo cha mkwewe lakini aligoma kuzungumza lolote na walipomwita kusogea eneo la kaburi mzee huyo hakukubali ndipo vijana hao walipoamua kufukia kaburi kisha kuubeba kinguvu mwili wa marehemu na kuhamishia katika kijiji cha Nungwe kwa wazazi wa marehemu ambako walichimba kaburi lingine na kutaka kuzika.

Aliongeza kuwa  kabla hayo yote hayajafanyika taarifa zilipelekwa Jeshi la Polisi ambao walifika eneo la tukio na kuwasihi watulie hadi Serikali itakapopima mwili wa marehemu ili kubaini ugonjwa uliomsababishia kifo na kisha kuamua ni upande upi unapaswa kuzika na siyo kung’ang’aniana mwili wa marehemu.

Baadhi ya ndugu wa marehemu walisema kitendo cha kuhamisha mwili wa marehemu haukufanywa na wao bali ni vijana waliokuwa wakichimba kaburi ambao hata wao hawakuhusishwa na ugomvi waliokuwa nao zaidi ya wao kuamrishwa kuondoka eneo la msiba na kuhamia kwao.

Mzee wa mila wa kijiji cha Dimbwe, Hezron Dimbwe alisema mwenye jukumu la kuzika ni upande wa wafiwa ambao ni ukoo wa mwanaume aliye muoa na si vinginevyo hivyo kama serikali itaamua wasizike Familia ya upande wa marehemu italizimika kulipa fidia kijijini kwa ajili ya kufukia kaburi.

Naye Mume wa Marehemu, Moses Pascal (27) mkazi wa Uyole Jijini Mbeya alisema mkewe alifikwa na umauti walipokuwa wameenda kijijini kwao Shilanga kwa ajili ya kilimo lakini kabla ya kifo cha Mkewe walikuwa wametoka Hospitali kumtibu mtoto wao majira ya saa Tisa alasiri.

Alisema baada ya kurudi nyumbani mkewe aliaga kwenda mtoni kufua hivyo alimwachia mtoto abaki naye lakini baada ya muda  kidogo akapata taarifa za kifo chake na kwamba alifanya juhudi za kwenda kumchukua hivyo hakukua na maongezo yoyote kabla ya kifo.

Akizungumzia kuhusishwa kwa baba yake na kifo hicho alisema ni maneno ya uzushi kutoka kwa watu na kwamba huenda anahusishwa kutokana na kubaki peke yake katika ukoo wao kutokana na wenzie wote kufa hivyo kuhusishwa na ushirikina.

Aliongeza kuwa bado baba yake anahusishwa kufuatia kifo chenye utata cha mtoto wake wa kwanza ambaye alifariki baada ya kumwagikiwa na maji ya uvuguvugu jambo ambalo pia baadhi ya watu walimtuhumu baba yake mzazi kuwa ni mshirikina.

Aidha hadi tunaingia mtamboni Mwili wa marehemu ulikuwa upo katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kwa ajili uchunguzi ili kubaini sababu ya kifo cha marehemu ili baada ya kupata majibu pande zote mbili zielezwe na kufafanuliwa na kukabidhiwa kwa taratibu za mazishi.

Na Mbeya yetu

No comments: