Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, September 25, 2013

WAENDESHA BODA BODA 300 WILAYANI RUNGWE WATUNUKIWA VYETI VYA UDEREVA PAMOJA NA LESENI.

Baadhi ya Pikipiki zinazoendeshwa na vijana Wilayani Rungwe waliotunukiwa vyeti na Leseni na Mkuu wa Wilaya hiyo Crispin Meela baada ya kumaliza mafunzo.
Afisa Biashara wa Wilaya ya Rungwe, Prince Mwakibete akisoma majina ya madereva wanaostahili kutunukiwa vyeti na mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispin Meela.  
Dereva wa Bodaboda Baraka Mwasile akisoma risala kwa niaba ya madereva wenzie kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwatunuku Vyeti na Leseni zao.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Noel Mahyenga akizungumza na Madereva wa bodaboda na kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ili akabidhi vyeti na Leseni.
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Crispini Meela akizungumza na Madereva wa bodaboda kabla ya kuanza kwa zoezi la kuwatunuku vyeti na leseni za kuendeshea pikipiki kwa vijana 300 wa Wilaya hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Rungwe akimkabidhi cheti dereva wa bodaboda kwa niaba ya wenzie 300 katika hafla iliyofanyika nje ya jengo la ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Tukuyu mjini.
Baadhi ya madereva wa Bodaboda wakifuatilia kwa makini zoezi la kutunuku vyeti lililokuwa likifanywa na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe.



IMEELEZWA kuwa mafanikio ya jambo lolote duniani  linatokana na kuwaelewesha vijana kwa kuwa ndilo kundi kubwa ambalo likisahaulika ni rahisi kupata matokeo tofauti na matarajio.

Hayo yalibainishwa jana na Mkuu wa Wilaya Rungwe Crispin Meela wakati wa Zoezi la kuwatunuku Vyeti na Leseni za kuendeshea pikipiki maarufu kwa jina la Bodaboda vijana 300 wa Wilaya ya Rungwe katika Hafla iliyofanyika katika Jengo la Halmashauri Tukuyu Mjini.

Meela alisema baada ya kugundua kuwa vurugu nyingi hutokea kutokana na vijana wengi kutokua kwenye makundi na shughuli maalumu za kufanya akaamua kuandaa mafunzo kwa Madereva wa Bodaboda ili wapate Leseni na vyeti ili wajue sheria za barabarani.

Alisema  baada ya kupatiwa mafunzo vijana hao tayari ni kundi maalumu ambalo limeshatambuliwa na ni rahisi kulisaidia kwa kuwaanzishia miradi mbali mbali itakayowasaidia kuepukana na vitendo viovu hasa vurugu zinazotokana na Siasa.

Alisema  kwa kuanzia atahakikisha Asilimia tano za Makusanyo ya mapato ya Halmashauri kwa ajili ya Mfuko wa Vijana zitasaidia kuanzisha Sacoss ambayo  kabla ya hapo watapatiwa elimu juu ya uendeshaji wake ikiwa ni pamoja na kuchagua viongozi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe,Noel Mahyenga alisema mradi wa Boda boda ni kichocheo kikubwa cha Wilaya hiyo baada ya vijana wengi kujishughulisha na kuwa tayari kuchangia shughuli za maendeleo ndani ya Wilaya.

Aliongeza kuwa tayari Halmashauri imeshapata kundi la Vijana ambalo limejikusanya pamoja hivyo itarahisisha kuwawezesha na kuwapatia msaada kutokana na kuachana na kazi zisizo rasmi.

Na Mbeya yetu


No comments: