Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, September 30, 2013

MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA MBEYA. DR. MARY MWANJELWA(CCM), AWACHANGIA LAKI TANO MASHABIKI WA TAWI LA MWANJELWA ENEO LA KABWE




 Juu na chini, Dr. Mary Mwanjelwa akipandisha bendera katika tawi hilo la Mwanjelwa ambako mashabiki wa timu ya Mbeya City, walimwalika kuwa mgeni rasmi.

 Viongozi wa Jiji la Mbeya wakishangilia ilipokuwa ikipanda bendera....
 Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya, Mussa Zungiza, akizungumza katika hafla hiyo fupi ya uzinduzi wa tawi la wakereketwa wa timu ya Mbeya City.
 Kulia ni Mwenyekiti wa mashabiki wa Mbeya City FC, Willy Mastala, akifurahia baada ya kukabidhiwa fedha taslmi Tsh. 500,000 na Mbunge wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa.



 Mbeya City hoyeeeeee..hoyeeeeee...hoyeeeee
 Mashabiki wa tawi la Mbeya City wakiwa pamoja katika hafla hiyo...
 Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, akielea protocal za kiuongozi, jambo ambalo vijana walionekana kutomwelewa huku wakipiga kelele za kutofurahia, baadae wakamshangilia baada ya kusema kuwa Jiji litawasafirisha mashabiki kuelekea Arusha tmu hiyo itakapoenda kucheza huko...
 Mbunge Dr. Mary Mwanjelwa akiwa ndani ya uzi wa MBEYA CITY






MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mbeya, Dr. Mary Mwanjelwa, amewachangia Sh. 500,000 mashabiki wa timu ya Mbeya City, walioamua kujiunga na kufungua tawi lao katikati ya Jiji la Mbeya.

Pesa hizo alizikabidhi juzi kwa mashabiki hao ambao walimwalika kuwa mgeni rasmi wa kufungua tawi la mashabiki wa timu hiyo kutoka eneo la Mwanjelwa na Kabwe.

Dr. Mwanjelwa alisema kuwa, timu ya Mbeya City imewauganisha na kutaka tawi hilo, liwe chachu ya umoja na mshikamano kwasababu huwezi kuzungumza Mbeya bila kutaja Mwanjelwa.

Mwenyekiti wa mashabiki hao, Willy Mastala, alisema tayari tawi lao lina akiba ya Sh. 450,000 na mashabiki hao wamejipanga kusafiri na kushangilia timu hiyo popote itakapoenda na gharama zote waliomba ziwe juu ya Jiji la Mbeya.

Meya wa Jiji la Mbeya, Athanas Kapunga, alisema kuwa Jiji lake litasafirisha mashabiki wote na bajeti ya timu hiyo tayari ipo na kwamba amefurahi kusikia kuwa Mbunge Mwanjelwa atakuwa mlezi wa tawi hilo.

Mkurugenzi wa Jiji hilo Mussa Zungiza, alisema kuwa anajisikia furaha kuona mashabiki wanaendelea kuunga mkono jitihada za Jiji lake kuimarisha timu ya Mbeya City.

Habari kwa hisani ya Kalulunga Media

No comments: