Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, July 18, 2013

WANANCHI WA KAPUNGA WILAYANI MBARALI WAGAWANYIKA KISA MWEKEZAJI.

Wananchi wakiendelea na ujenzi wa shule ya kijiji 
Wananchi wakishusha shehena ya saruji iliyonunuliwa na wananchi
Mwenyekiti wa kijiji cha Kapunga Ramadhani nyoni mwenye suti akikagua daftari  la vifaa vilivyo pokelewa 
Walimu wakikagua Daftari za mahudhurio ya wanafunzi 
Mwenyekiti wa kijiji cha Kapunga kushoto akipokea taarifa kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi ya Kapunga 
Afisa Elimu Wilaya ya Mbarali Benedict Kibodya   aliyevaa kizibao akikagua ujenzi wa shule 
Wanafunzi wa shule ya msingi Kapunga wakicheza  huku ujenzi ukiendelea 
Majengo yaliyo kabidhiwa na Mwekezaji kwa Halmashauri ya Wilaya 
Watoto waliofika shuleni hapo bila kuwepo walimu 
Mandhari ya shule iliyojengwa na Mwekezaji
Wanafunzi wakivuka katika Nguzo bila kujali hatari ya Mfereji 



Wakazi wa Kijiji cha Kapunga na Wananchi wa Kitongoji cha SiteOne wote wa Kijiji cha Kapunga Wilaya ya Mbarali Mkoa wa Mbeya, wamejikuta wakigawanyika baada ya Mwekezaji wa Kapunga Rise Project kujenga Shule ya Msingi kwa ajili ya Matumizi ya Kijiji hicho lakini kukataliwa na kujenga ya kwao.

Mgawanyiko huo umetokea baada ya Wananchi wa Kijiji hicho kukataa kuyatumia madarasa yaliyojengwa na Mwekezaji na baadaye kujenga madarasa mengine ambayo yameanza kutumika huku baadhi ya Wakazi wa Kitongoji cha SiteOne kugomea madarasa ya Kijiji na kutaka kutumia Majengo ya Mwekezaji.

Wananchi wa Kitongoji hicho wamesema hawako tayari kutumia madarasa yaliyojengwa na Wanakijiji licha ya madarasa yaliyojengwa na Mwekezaji kukosa miundombinu muhimu kama Madawati na Walimu na kuahidi kuchonga Madawati 75 ndani ya wiki hili kwa ajili ya Wanafunzi 151.

Hata hivyo hali bado itabaki katika Sintofahamu juu ya Walimu na Vitendea kazi vya kufundishia baada ya kumaliza kutengeneza madawati kutokana na Walimu waliokuwa wakifundisha Shule ya Awali kuhamia katika Shule ya Kijiji.

Wanakijiji waligomea kutumia Shule ya Mwekezaji ambayo ilikabidhiwa na Meneja wa Shamba hilo Justine Veemark kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gulam Hussein Kiffu katika hafla iliyofanyika Julai 5, Mwaka huu na kuhudhuriwa na Afisa Elimu wa Mkoa wa Mbeya Juma Kaponda, Viongozi wa Elimu ngazi ya Wilaya Mwenyekiti wa Kijiji pamoja na Wananchi.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho Ramadhani Nyoni amesema wameshindwa kuyatumia majengo hayo kutokana na kutopata maelekezo yoyote Serikalini kuhusu Wanafunzi wanaostahili kusoma katika Shule hiyo wakiwemo Walimu hali iliyowalazimu kujenga shule nyingine kwa manufaa ya watoto wao.
Aidha Mwenyekiti huyo anakiri kukabidhiwa funguo za shule hiyo lakini haitumiki licha ya Wanafunzi wanaotoka katika Kitongoji cha Site One kuhudhuria shuleni hapo kila siku na kuishia kucheza tu kutokana na kutokuwepo kwa madawati na walimu.

Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa mbali na kugomea kuyatumia majengo hayo pia hawakushirikishwa kabla ya kuanza kwa ujenzi na kumlaumu Mwekezaji kwa kubadili matumizi ya Shamba ambalo alipewa kwa ajili ya kilimo lakini yeye kujenga Shule ndani ya Shamba alilowekeza.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa Juma Kaponda amemshukuru mwekezaji huyo kwa kujenga shule nzuri na kumtaka kuongeza eneo kutoka Ekari 3.8 kufikia 7.5 ambapo mwekezaji amekubali kufanya hivyo.

Hata hivyo Kaponda amemshauli mwekezaji kuhamisha hati miliki ya eneo hilo la shule ili lihamie sasa kweye hati miliki ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali.

Afisa Elimu amesikitishwa na kitendo kilichofanywa na wazazi wa  Site One cha kuwapeleka wanafunzi bila kuwepo kwa walimu shuleni hapo na kwamba wanafunzi watakao soma shule iliyojengwa na mwekezaji ni  kuanzia darasa la kwanza hadi la sita kwani wale wa darasa la saba wamesha sajiliwa kwa ajili ya mitihani.

Aliongeza kuwa shule ya wanakijiji itatumia usajili wa zamani na hii mpya itapewa usajili mpya 

Picha Ezekiel Kamanga 
Mbeya yetu



No comments: