Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, July 22, 2013

WADAU WATOA CHANGAMOTO ZA MTANDAO WA MBEYA YETU.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Philip Saliboko, alipokuwa akichangia Mada katika Kongamano la Wandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya na Wadau lililofanyika katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya.



Katika kuonesha Mtandao wa www.mbeyayetu.blogspot.com unaendelea kutoa habari za kuaminika kote Ulimwengu baadhi ya Wadau wameshauri kujikita zaidi katika kutangaza vivutio vinavyopatikana ndani ya Mkoa wa Mbeya ili kuvutia Watalii na wawekezaji kuja Mkoani Mbeya kuwekeza na kuongeza uchumi na maendeleo ya Mkoa.

Rai hiyo imetolewa jana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Philip Saliboko, alipokuwa akichangia Mada katika Kongamano la Wandishi wa Habari Mkoa wa Mbeya na Wadau lililofanyika katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya.

Saliboko amesema kutokana na teknolojia kubadilika watu wengi hupendelea  kusoma mitandao ya kijamii ambayo husomwa sehemu kubwa duniani hivyo yanapoandikwa mambo mazuri ya Mkoa wa Mbeya yatasaidia katika kuinua maendeleo na uwekezaji wa Mkoa na Taifa kwa ujumla.

Ametolea mfano mtandao wa Mbeya yetu kuwa ukitangaza na kuandika habari za vivutio vya utalii vinavyopatikana ndani ya Mkoa itasaidia kuwavuta watalii wa kimataifa kufika na kutembelea vivutio hivyo na hatimaye kyuimarisha utalii wa ndani ya Mkoa wa Mbeya.

Aidha kwaupande wake Uongozi wa Mtandao huo katika kujibu changamoto hiyo, wamekubaliana na ushauri huo na kutoa Wito kwa Wadau wa Maendeleo wa Mkoa wa Mbeya kuwasaidia namna ya kuvifikia na kupata historia za Vivutio hivyo ili viweze kutangazwa.

Hata hivyo wamedai kuwa suala linaloukabili Mtandao huo ni kutokana na ukosefu wa miundombinu mizuri itakayoweza kuwafikisha Waandishi wake katika Maeneo mbali mbali ambapo wametoa Wito kwa Halmashauri zote kusaidia kuwawezesha kuvifikia vivutio vya utalii katika maeneo yao.

No comments: