Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, July 26, 2013

TBL YAKABIDHI KISIMA CHA SH. MILIONI 28 KIJIJI CHA ISNURA, MBARALI, MKOANI MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gulam Kiffu kulia na Meneja kampuni ya bia (TBL) Nicolaus Kanyamala wakizindua kisima cha kijiji cha Isnura 
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gulam Kiffu akimtwisha maji mwenyekiti wa kijiji cha isnura Josephine ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa kisima hicho
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Gulam Kiffu akiwashukuru TBL kwa kusaidia maji katika kijiji cha isnura na kuahidi kukitunza kisima hicho
Meneja uhusiano wa TBL Dorris Malulu akizungumza na wakazi wa Isnura ambapo amesema kuwa TBL imekuwa na sera ya kusaidia maeneo mbali mbali hapa nchini kupitia faida kidogo inayopata kwa kuamua kurudisha sehemu ya faida hiyo kwa wananchi baada ya kubaini uhitaji wa msaada eneo husika, ambapo pamoja na mambo mengine meneja huyo alitoa rai kwa jamii kuona umuhimu wa kuisaidia serikali hapa nchini.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Isnura  Josphine Ndimilage akisoma risala kwa niaba ya wananchi
Uchimbaji wa kisima katika Kijiji hicho umefadhiliwa na Kampuni ya Vinywaji ya Tbl kwa gharama ya Shilingi milion 28  ikiwa ni pamoja na Jenereta ndogo kwa ajili ya kupandisha maji katika Tanki kubwa lenye ujazo wa Lita 45,000.

Picha na Mbeya yetu


No comments: