Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Monday, June 24, 2013

WATUMISHI wa Shirika la Umeme Nchini( Tanesco) wameaswa kufanya kazi zinazohusu Shirika hilo pekee na siyo kujihusisha na kazi za Ukandarasi, hali inayosababisha mgongano wa Maslahi kato yao na Wakandarasi. Mbeya

Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mbeya katikati Injinia Amos Maganga katika Mkutano wa Uongozi wa Tanesco Mkoa wa Mbeya na Wamiliki wa Makampuni ya Ukandarasi wa Umeme na wanachama wa Chama cha Wakandarasi wazawa Tanzania wa Mkoa wa Mbeya (TLCO) uliofanyika katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya.
Baadhi ya wakandarasi wa mkoa wa Mbeya wakimsikiliza meneja wa Tanesco mkoa wa Mbeya



WATUMISHI wa Shirika la Umeme Nchini( Tanesco) wameaswa kufanya kazi zinazohusu Shirika hilo pekee na siyo kujihusisha na kazi za Ukandarasi, hali inayosababisha mgongano wa Maslahi kato yao na Wakandarasi.


Aidha imeelezwa kuwa Mtumishi atakayebainika kujishughulisha na kazi ambazo zinatakiwa kufanywa na Mkandarasi ajitoe kabisa katika Shirila ka Tanesco ili aendelee na kazi hiyo ambapo pia Wakandarasi wanajiingiza katika Shughuli za Tanesco pia wameatakiwa kuacha.
  
Agizo hilo lilitolewa  na Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mbeya Injinia Amos Maganga katika Mkutano wa Uongozi wa Tanesco Mkoa wa Mbeya na Wamiliki wa Makampuni ya Ukandarasi wa Umeme na wanachama wa Chama cha Wakandarasi wazawa Tanzania wa Mkoa wa Mbeya (TLCO) uliofanyika katika ukumbi wa Mkapa Jijini Mbeya.
  
Aidha katika Mkutano huo ambao awali Raisi wa Chama cha Wakandarasi Wazawa Tanzania (TLCO) Kura Mayuma, alisema Tanesco na Wakandarasi ni wadau muhimu wa kumsaidia Mwananchi lakini wanashindwa kufikia mwafaka kutokana na kuwepo kwa Changamoto.
  
Alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na kutokuwa na Mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi na Watumishi wa Tanesco, Watumishi wa Tanesco kufanya kazi za Umeme sambamba na wakandarasi ambapo alisema  Chama kimepata malalamiko kuwepo kwa watumishi ambao huchukua na kufanya kazi za kikandarasi.

Alisema kutokana na kuingiliana huko kunawafanya Wakandarasi kuishi maisha ya kuviziana kwa kuwa wateja wengi hasa vijijini humwamini zaidi Mtumishi wa Shirika kuliko Mkandarasi ambaye ndiye mwenye jukumu la kutengeneza umeme.

Changamoto zingine ni Vifaa vya kufanyia kazi kutotosheleza, Mamlaka zingine za Kiserikali kama Tamesa, Nhc, Wakala wa majengo, Halmashauri za Wilaya, Manispaa na Majiji kufanya kazi za Wakandarasi, upimaji wa Service line kuwa na kasoro, Vishoka, kutotambuliwa kwa Wakandarasi na ofisi ya Tanesco.
  
Zingine kutokupewa kazi za kusambaza  umeme (kujenga service line), upendeleo wa ajira, kitengo cha umeme wa dharula kuchelewa kufika eneo la tukio na  Malalamiko ya wateja kuwa Shirika haliwamilikishi moja kwa moja wateja mali wanazolipia.
  
Kwa upande wake Meneja wa Tanesco Mkoa wa Mbeya Injinia Amos Maganga, alikijibu baadhi ya Changamoto hizo alisema Tanesco na Wakandarasi wote kwa pamoja wanadhana moja ya kuhakikisha mteja wanatendewa haki.

Alisema ili kurudisha mahusiano mazuri kati ya Watumishi wa Tanesco na  Wakandarasi ni pamoja na kukutana mara kwa mara kwa kufanya mikutano ambapo katika Mkutano huo iliadhimiwa kukutana kila baada ya miezi 6.
  
Maganga aliongeza kuwa Mahusiano pia yatakuwepo endapo Mkandarasi atafanya kazi yake bila kuingilia majukumu ya Tanesco kama vile Watumishi wa Tanesco kutengeneza umeme hadi kwenye mita na siyo kuingia ndani ya nyumba ya mteja.

Pia alisema Wakandarasi hawaruhusiwi kupanda kwenye nguzo na kugusa mita kwa kuwa jukumu hilo ni la wataalamu wa Tanesco na kuongeza kuwa iwapo Mkandarasi atakutwa kwenye nguzo atachukuliwa hatua kama kishoka wa umeme.

Alisema baadhi ya Wakandarasi kuhusishwa na wizi wa Umeme ambapo baada ya kukamatwa kwa wezi huwataja wao, pia kupitisha kazi zisizokuwa na sifa, Mihuri yao kutumika vibaya na kujengwa laini zisizohalali na kupitishwa na Mkandarasi  bila kupitia taarifa Vizuri.

Aliongeza kuwa Changamoto nyingine inayofanywa na Makandarasi ni ulanguzi wa Fomu ya Maombi ya mteja ambazo huziuza kati ya Shilingi 50,000/= na 80,000/= ili hali bei hali ni Shilingi ni kati ya 6000/= na 10,000/=.

Hata hivyo kutokana na kukithiri kwa hali hiyo Meneja huyo alisema baadhi ya Wakandarasi wameacha kazi zao na kujishughulisha na ulanguzi wa Fomu hivyo kuagiza kuwa Mkandarasi hata husika na kumchukulia fomu mteja.

“ Kuanzia leo nasema Mteja akiwa na picha yake atanunua fomu ndipo atakapomtafuta Mkandarasi kwa ajili ya taratibu zingine maana hii tabia imesababisha hata fomu kuisha mapema kutokana na baadhi yao kuhodhi fomu nyingi na kuzunguka kwenye makorido ya Ofisi za Tanesco ili kuvizia wateja” alisema Meneja huyo.


Aidha aliwahimiza Wakandarasi kuheshimu ofisi zao kwa kutulia na kusubiri wateja na siyo kuwavizia wateja kwa kuwalangua bei ya Fomu na kumlazimisha kumfanyia kazi.

Na Mbeya yetu

No comments: