Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, March 6, 2013

WALEMAVU WATAKA UWAKILISHI KWA KUCHAGULIWA


CHAMA cha watu wenye ulemavu (CHAWATA) mkoani Mbeya kimependekeza katiba ijayo iruhusu wawakilishi wa walemavu katika ngazi ya halmashauri na bunge wapatikane kwa kupigiwa kura.  Mapendekezo hayo yametolewa na wajumbe waliohudhuria mdahalo wa kuwajengea uwezo walemavu kuchambua katiba ya nchi ya sasa na kuibua mapendekezo ya kuingizwa kwenye katiba mpya uliofanyika katika ofisi za chama hicho jijini hapa kwa ufadhili wa shirika la The Foundation For Civil Society. Mmoja wa wajumbe hao Willium Simwali kutoka wilayani Mbeya amesema mfumo uliopo sasa wa rais kuteua mwakilishi wa jamii ya walemavu bungeni hautoi demokrasia badala yake mwakilishi huyo alipaswa kupatikana kwa kupigiwa kura. Simwali amesema vyama vya watu walio na ulemavu ndivyo vinapaswa kushiriki mchakato wa kutafuta mwakilishi kuanzia katika ngazi za mitaa kwa kila kimojawapo kutoa mgombea na kumshindanisha na vyama vingine vya watu wa jamii hiyo. Naye Isaya Kyando kutoka Mbozi ametaka katiba ijayo itoe maelekezo ya vifaa kwaajili ya walemavu kuuzwa kwa bei zitakazowawezesha kumudu kununua na pia serikali kuwa na fungu kwaajuili ya kuwawezesha watu wa jamii hiyo hususani kwa kuwanunulia vyombo vya usafiri. Mwenyekiti wa Chawata mkoani hapa Jimmy Ambilikile amesema mdahalo huo umehudhuliwa na wajumbe wawakilishi kutoka wilaya zote za mkoani hapa ambao licha ya kutoa maoni yao pia watapeleka mrejesho wa wanachama watakaporejea wilayani kwao



Kwa hisani ya Joachim Nyambo 

No comments: