Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, January 8, 2013

UKARABATI WA KITUO CHA MABASI WILAYANI MBEYA VIJIJINI MBALIZI WASUASUA

STENDI ya mabasi ya Wilaya ya Mbeya Vijijiji iliyopo eneo la Mbalizi mkoani Mbeya, ukarabati wake unasuasua wakazi wengi wa mji huo mdogo wa mbalizi wameiomba serikali kukamilisha kituo hicho mapema kwani tayari mvua zimeanza kunyesha na kuwa kero kubwa katika eneo hilo
Hii ndiyo hali halisi iliyojionea mbeya yetu katika pitapita zake za maeneo hayo ya mbalizi
Ukarabati wa standi hii ya Mbalizi unakuja ikiwa ni miaka mitatu tu tangu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Kikwete kuahidi kuikarabati Stendi hiyo baada ya kujionea na kusikiliza kilio cha wananchi waliokuwa wamrjitokeza kumskiliza akijinadi katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010.
Ni kipande kidogo tu mpaka sasa kimekarabatiwa katika kituo hicho cha mbalizi

Je tutapona na magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu?


picha na Mbeya yetu

No comments: