Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, September 22, 2012

BAADA YA NCHI JIRANI MWANAMKE KUZAA NA BABA YAKE WATOTO WATATU, SASA HUKU MBEYA BABA MZAZI (39) AMPA MIMBA MWANAE WA KUMZAA MWENYE UMRI WA MIAKA 15


Habari na Ezekiel Kamanga,Mbeya.
 Mkazi wa Mtaa wa Mbete,Kata ya Isanga Jijini Mbeya Bwana Yussuf Hamad(39),anatuhumiwa kumpa mimba binti yake wa kumzaa(15) jina lake limehifadhiwa.

Hayo yamethibitishwa na Mama mzazi wa binti huyo Bi, Regina Simon(35) baada ya kupata taarifa Mei 11 mwaka huu kuwa binti yake ana ujauzito wa miezi minne,na kuamua kutoa taarifa kwa Balozi  wa mtaa huo Bwana Steven Ovaova ambaye naye alitoa taarifa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji Bwana Angelo Sanga.

Viongozi hao wa mtaa walimuita  mtuhumiwa na ili kupata ukweli wa tukio hilo,lakini mtuhumiwa alikanusha ingawa binti yake alithibitisha kutendewa ukatili huo na kwamba alikuwa akitishiwa kwa mapanga kila alipokuwa akifanya naye tendo la ndoa.

Baada ya uongozi kupata maelezo kutoka kwa binti huyo na mzazi kukataa waliamua kuipeleka kesi hiyo Polisi,ambapo walitoa PF3 iliyomwezesha binti huyo kupelekwa kwa daktari ambaye alithibitisha kuwa binti huyo ana ujauzito.

Hata hivyo hivi sasa binti huyo amelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mbeya akisubiri kujifungua ingawa umri mdogo wa binti huyo amekuwa chini ya uangalizi wa karibu wa daktari hospitalini hapo.

Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani Septemba 25 mwaka huu katika mahakama kuu jijini hapa,ili kujibu tuhuma zinazomkabili kesi inayotarajiwa kusikilizwa na hakimu wa mahakama hiyo mheshimiwa Majige.

No comments: