Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, August 31, 2012

WATANO WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMFANYIA FUJO DC MBARALI MBEYA


SAKATA la MKUU wa Wilaya ya Mbarali Gulamu Hussen Kiffu  kunusurika kuumizwa na wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Chimala kilichopo Wilayani humo mkoani Mbeya baada ya kuvamia gari lake na kuvunja vioo,kutoa upepo wa matairi  kutokana na Serikali kufunga chuo hicho kwa kutokuwa na hadhi ya kudaili wanafunzi, watu watano wamefikishwa mahakamani.

Kutokana na vurugu hizo zilizotokea chuoni hapo jana jioni, Jeshi  la polisi Mkoani Mbeya linawashikilia wanafunzi  sita    akiwemo Mkuu wa Chuo  hicho  Francis Mtega  kwa  tuhuma za kuhamasisha vurugu  zilizopelekea  kuharibu gari la Mkuu wa Wilaya ya  Mbarali. 

Kamanda wa polisi Mkoani hapa Diwani Athuman  alisema  baada ya mkuu wa wilaya kuongozana na baadhi ya viongozi wa serikali  hususani kamati ya ulinzi na usalama wilaya kwa lengo la kutaka kujua sababu za chuo hicho kuendelea kufundisha wakati serikali ilitoa agizo kifungwe ndipo hapo walipovamiwa na wanachuo hao.

Alisema   tukio hilo lilitokea muda mfupi baada ya kuwasili Chuoni hapo kwa  lengo la  kuzungumza na uongozi wa chuo ndipo baadhi ya wanafunzi  walivamia gari la Mkuu wa Wilaya na kuanza kuvunja vioo kwa kutumia mawena kisha kutoa upepo kwa malengo yasiyojulikana.

Kamanda Athumani alisema tukio hilo linaonesha ni mpango uliokuwa umepangwa na uongozi wa Chuo  kwa muda mrefu kwani serikali ina malengo mazuri kwa watanzania  na lengo kuu ilitaka chuo hicho kisajiliwe  ili kitambulike  na Serikali na kuweza kutoa wauguzi walio na sifa na kuwawezesha kupata ajira itakayotambulika serikalini. 

Aliongeza kuwa  kitu cha kushangaza ni madaraka aliyonayo mkuu wa chuo hicho ambapo yeye mwenyewe ni mwalimu na mhasibu na kwamba kulikuwa hakuna sababu ya kufanya vurugu bali  kilikuwa ni kitu cha kutoa vielelezo vya udaili wa chuo.

Alisema katika uchunguzi wa awali  umebaini kuwa chuo hicho kimeanza muda mrefu na tayari  kimeweza kutoa wauguzi katika Nyanja mbalimbali  bila ya serikali kutambua  kama hakijasajiliwa na hakitambuliki.

Kwa hisani ya Venance Matinya, Mbeya.


1 comment:

Anonymous said...

Mpaka chuo kinatoa wahitimu, wahusika/serikali ilikuwa wapi? viongozi wa mitaa, kata, wilaya, tarafa na wilaya walikuwa wapi?

Watu wanafanya mizaha hadi kwenye fani ya afya. Ni hatari sana. Kweli ccm imechoka.