Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Friday, April 27, 2012

WANANCHI WAMUOMBA MKUU WA MKOA KUTATUA MGOGORO WA KUTENGULIWA MWENYEKITI WA KIJIJI - MBEYA


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Abass Kandoro 
*******
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbarali.
Wananchi wa Kijiji cha Ijumbi, Kata ya Ruiwa Wilaya ya Mbarali Mkoani Mbeya, wamemuomba Mkuu wa Mkoa Bwana Abbas Kandoro kuingilia kati mgogoro baina ya pande mbili zinazopingana Diwani na Afisa Mtendaji wa Kata wakidaiwa kumuengua Mwenyekiti wa kijiji hicho kwa kutumia madaraka yao.

Kauli hiyo imetolewa na wananchi wa Kata hiyo kawa nyakati tofauti wakati wakiongea na mtandao huu kijijini hapo, ambapo inadaiwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana John Kalikumoyo ameenguliwa uongozi  kutokana na ubadhilifu pia kuitisha mikutano ya hadhara bila kibali na kuzuia wananchi katika shughuli za maendeleo.

Wananchi hao wamepinga madai hayo na kuwa ni njama za mtendaji Kata Bwana Jordan Masweve na Diwani mheshimiwa Alex Mdimilage, kwani ya kudhoofisha juhudi za mwenyekiti huyo kwa kuzuia mianya ya upatikanaji wa pesa kinyume na utaratibu wa makusanyo ya pesa za serikali.

Imedaiwa kuwa Viongozi hao wa kata waliitisha mkutano wa halmashauri ya Kijiji Aprili 17 mwaka huu, wakimtuhumu Bwana Kalikumoyo kwamba ameuza ng'ombe aliyekamatwa kijijini hapo na kujipatia fedha jumala ya shilingi milioni 1,080,000 na makosa hayo yanafanya kupoteza sifa za kuwa kiongozi.

Aidha viongozi hao walimtaarifu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali na yeye kuandika barua Aprili 18 mwaka huu, kutengua uongozi wa uenyekiti wa kijiji na kumkaimisha Afisa Mtendaji wa Kijiji.

Katika sakata hilo wananchi wa kijiji hicho wamemuomba Mkuu wa Mkoa Bwana Kandoro, kwenda haraka iwezekanavyo kijijini hapo ili kuleta suluhu kwani wananchi hao wamedai kuwa viongozi hao wa kata Bwana Masweve na Mdimilage ndio wabadhilifu.

Hata hivyo miongoni mwa vitendo vinavyolalamikiwa na wanachi kwa viongozi hao ni pamoja na kujipatia zaidi ya shilingi milioni 24 kutoka kwa wafugaji ambazo hazijaingia katika mfuko wa kijiji, ba kwamba suala hili Mkuu wa mkoa anapaswa kuunda tume ya kuchunguza kwani hawapo tayari kuchangia shughuli za maendeleo kama vile ujenzi wa shule za sekondari, zahanati na maji.

Wakati huo huo wamesema sababu yao ya kutka kususia kuchangia shughuli za maendeleo ni kutokana na viongozi hao kukataa kusoma bajeti ya mapato na matumizi ya kijiji, na badala yake kuwataka viongozi wa Vijiji kusoma taarifa hizo, hali inayowapelekea kuwa na swali kuwa Serikali ya kata haina mapato na matumizi?.

Baadhi ya vijiji vinavyohusishwa kutumiwa na Viongozi hao wa kata ni Motomoto, Malamba, Mahango, Igalako na Udindilwa vyote vilivyopo katika Kata ya Ruiwa.

No comments: