Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Tuesday, February 7, 2012

ATHARI ZILIZOJITOKEZA BAADA YA MWEKEZAJI WA KAPUNGA RICE PROJECT KUMWAGA SUMU.

Mguu ya Bwana Benjamini Hebel (44) mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Kapunga, wilaya ya Mbrani mkoa wa Mbeya ilivyoharibika baada ya Mwekezaji wa Kapunga Rice Project Bwana Wally Vermaak. kumwaga sumu kwa kutumia ndege katika mashamba ya wananchi kufutia mgogoro wa kugombania ardhi baina ya wananchi na mwekezaji huyo.
Baadhi ya wananchi walioathirika na Sumu iliyomwagwa na Mwekezaji Bwana Wally Vermaak. katika mashamba yao, na kisha kula mboga iliyomwagiwa sumu, hali iliyopelekea kuhara.
Kibanda hiki nacho kilimwagiwa sumu na mwekezaji wa Kapunga Rice Project Bwana Wally Vermaak. licha ya wananchi kujihifadhi ndani ya kibanda hicho.
Sehemu ya mimea ya mpunga na mahindi iliyonyauka katika mashamba ya wananchi wa Kijiji cha Kapunga baada ya kumwagiwa sumu na Mwekezaji wa Kapunga rice Project Bwana Wally Vermaak. .
Sehemu ya mimea ya mahindi iliyonyauka katika mashamba ya wananchi wa Kijiji cha Kapunga baada ya kumwagiwa sumu na Mwekezaji wa Kapunga rice Project Bwana Wally Vermaak..
Mtoto huyu alikuwepo shambani wakati mwekezaji akimwaga sumu mashambani.
Sehemu ya mimea ya mpunga na mahindi iliyonyauka katika mashamba ya wananchi wa Kijiji cha Kapunga baada ya kumwagiwa sumu na Mwekezaji wa Kapunga rice Project Bwana Wally Vermaak..
Sehemu ya mimea ya mpunga na mahindi iliyonyauka katika mashamba ya wananchi wa Kijiji cha Kapunga baada ya kumwagiwa sumu na Mwekezaji wa Kapunga rice Project Bwana Wally Vermaak.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Kapunga Bwana Ramadhani Nyoni akionesha turubai ambalo lilitumika kufunika mbegu na kisha kunyunyiziwa sumu ambayo iliharibu turubai hilo na mbegu. (Picha na Ezekiel Kamanga).

No comments: