Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, January 25, 2012

SERIKALI YATAKIWA KUACHA POROJO KUHUSU UTEKELEZAJI WA AHADI KUHUSU WAZEE

  MWENYEKITI WA TUWATA MKOA WA MBEYA LYDIA NJENI AKISISITIZA JAMBO KATIKA KONGAMANO
 KATIBU MKUU WA TUWATA DK. DAVID MAGOGO AKIZUNGUMZA KATIKA KONGAMANO HILO
 MZEE JAMES SILINJANJE MWOLO (76) MKAZI WA MAJENGOJIJINI MBEYA

SERIKALI iliyopo madarakani imetakiwa kuacha porojo kwenye majukwaa kuhusu kutoa huduma kwa wazee nchini kwani kwa kufanya hivyo ni kujichimbia kaburi siku za usoni

Wakizungumza katika Kongamano la Wazee lililoandaliwa na Asasi isiyo ya Kiserikali ya Tumaini La Wazee Tanzania (TUWATA) ambalo limefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Catholic Youth Centre Jijini Mbeya wamesema serikali imefikia hatua ya  kuwasahau wazee amabao kwa uhalisia wameiweka serikali madaraka.


Mzee aliyejitambulisha kwa jina la James Silinjanje Mwolo (76) mkazi wa Majengo Jijini Mbeya kwa uchungu mwingi amesema tangu mfumo wa vyama vingi uanze nchini Tanzania suala la wazee halijatiliwa maanani hata kidogo ukilinganisha na enzi za Mwalimu Nyerere.

Ameongeza kusema wakati akiwa kama Mhandisi wa Vyuma daraja la Pili kulikuwa na haki ambazo wazee walikuwa wakipewa kutoka serikalini kama tiba na chakula tofauti na ilivyo sasa.

Wazee wengine kwa ujumla wao wamesema serikali imewatupa hususani katika suala la tiba wafikapo hospitali  usumbufu umekuwa mkubwa, wengine wakilazimishwa kutoa pesa kidogo ili waweze kupewa huduma kwa haraka zaidi hali ambayo wameiita ni “matusi” kwa serikali ya Chama cha Mapinduzi.

Pia wazee hao wamesema inashangaza kuona serikali imetilia mkazo zaidi kwa watoto huku ikiwasahau wazee bila kujua ama kwa kujua kuwa baadaye  watafikia hatua ya kuwa wazee, na ambao hawawalei watoto wengine wamefunguliwa mashtaka kutokana na kosa hilo.

Wazee hao kwa uchungu mwingi wamesema  kungekuwepo pia sheria ya kuwabana wasiowatunza wazee ili haki itendeke nchini.

No comments: