Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Thursday, November 24, 2011

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA BAADA YA NYUMBA ALIYOKUWA AKIISHI KUCHOMWA MOTO NA WATU WASIOJULIKANA MKOANI MBEYA.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi.
*****
Na mwandishi wetu
Mkazi mmoja wa Mbambo wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya Lastoni Mwangosi anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 40 hadi 50 amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kuchomwa moto na watu wasiofahamika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi amesema Bwana Mwangosi amefikwa na mauti jana majira ya saa 1 usiku baada ya nyumba yake kuchomwa moto.

Hata hivyo Kamanda Nyombi amemaliza kwa kusema chanzo cha mauaji hayo ni imani za kishirikina na Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kubaini aliyehusika na tukio hilo .

No comments: