Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Saturday, October 22, 2011

KIJANA MMOJA ALIYEHITAJI MSAADA WA MAZISHI, AFANYA UTAPELI NA KUTOKOMEA KUSIKOJULIKANA



Afisa mtendaji wa mtaa wa Maendeleo kata ya Iyunga jijini Mbeya Bi Tabu Sengo Tabu ambaye ametapeliwa simu yekye thamani ya shilingi 90,000/= kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Geogre Ramsi aliyedai kuwa ametokea jijini Tanga,  alifika katika uongozi wa serikali hiyo kuomba msaada wakumzika ndugu yake aliyedaiwa amejifungua na kufariki katika Hospitali ya Rufaa Meta jijini hapa.
 Bwana Elias Mwakyusa aliyeitwa kusaidia kuzika akiwa amefika kwa fundi seremala kubeba misalaba.
 Dereva akiwa na pikipiki iliyokodiwa na kijana tapeli George Ramsi aliyedai kufiwa na ndugu yake aliyejifungua katika hospitali ya Rufaa Meta kwa njia ya operasheni ambaye naye alitapeliwa simu yenye thamani ya shilingi 80,000/= za kitanzania na fedha zilizokuwa katika akaunti ya MPESA shilingi70,000/=
Fundi seremala Bwana Maiko Mwakalonge aliambiwa  atengeneze misalaba yenye thamani ya shilingi 10.000/= na kijana tapeli George Ramsi ambapo hakuweza kulipwa.
 Gari iliyokodiwa na kijana tapeli George Ramsi kwa shilingi 20,000/= kwa ajili ya kuwabeba wachimbaji wa kaburi wanne(majina yao katika habari inayofuata chini), ambapo umbali hadi kufikia eneo la makaburi ni kilometa 5 kutoka Iyunga.

Vijana wa kutoka kushoto ni Obadia Robert Kyando, Obby Mwakasasagule, Shida Mwasambili na Matatizo Kyando waliokodiwa kwa ajili ya kuchimba kaburi kwa shilingi 110,000/= ambapo waliahidiwa kulibwa na kijana huyo baada ya mazishi lakini hawakuweza kulipwa.
Fundi seremala Maiko Mwakalonge aliyefika katika ofisi ya Afisa mtendaji Bi Tabu Sengo kutoa malalamiko ya kutengeneza misalaba na mteja wake kutoonekana.

Kijana huyo tapeli George Ramsi ametokomea kusikojulikana baada ya kupelekwa kwa Mchungaji wa kanisa la Sabato Nzovwe, majira ya saa saba akiomba taratibu za mazishi kufanyika katika kanisa lake, kitu ambacho si cha kweli na kudai anaomba kwenda kununua vocha ndipo alitokomea moja kwa moja na simu ya afisa mtendaji, dereva wa pikipiki na shilingi elfu mbili ya dereva taksi.

Hata hivyo baada ya kijana huyo kutofika makaburini ndipo kulipopelekea kupatikana kwa taarifa za kuwa kijana George ni tapeli na taarifa zilipelekwa katika Kituo cha polisi cha Iyunga.

1 comment:

Anonymous said...

Ilikuwaje hao jamaa wakatoa cmu kwa mtu wasiyemjua....!!? Kama vipi Kuna uzembe ndani yake, sasa kazi kwao kusaidiana na polisi kumsaka jamaa..!! NA kusisitiza polisi jamii kwenye maeneo Yao...!! Nawapa pole sana kwani jamaa kawarudisha nyuma...!!