Social Icons

Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com

bre

Wednesday, September 7, 2011

WANAFUNZI KUWA NA UMRI MDOGO KWA CHANGIA,KUPUNGUA KWA UCHANGIAJI DAMU SALAMA MKOANI MBEYA.

Picha hii ni kielelezo cha jinsi ya uchangiaji damu.
Na mwandishi wetu.
Uchangiaji wa damu salama mashuleni mkoani Mbeya umepungua kutokana wanafunzi wanaochanguliwa kujiunga na masomo ya sekondari kuwa na umri mdogo na hivyo walio wengi kukosa kutimiza vigezo vya uchangiaji damu ambapo kigezo mojawapo ni kuanzia umri wa miaka 18.

Akiongea na mwandishi wetu Meneja wa kitengo cha damu salama nyanda za juu kusini Daktari Lelo Bilihima amesema kuwa licha ya kampeni na juhudi zinazofanywa na kitengo hicho kuwa uhitaji wa damu unatakiwa kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na kiasi kilichopo katika hospitali nyingi.

Aidha ameongeza kuwa damu hiyo haiuzwi na kwa yeyote atakayebainika anauza damu hiyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Wakati huo huo akizungumzia upande wa wananchi Dkt. Baliyima Lelo amesema kuwa wachangiaji wengine wanaogopa ukubwa wa sindano hivyo kupunguza uchaangiaji wa damu na amewataka wananchi kuondokana na uvumi ulioenea kwa sasa kuwa mchangiaji akichangia mara moja atatakiwa kuchangia tena kwa zaidi ya mara na kusisitiza kuwa jukumu la kuchangia damu ni wajibu wa kila mmoja.

No comments: